Kumuoa Mkristo Atakayesilimu Siku Ya Ndoa
 SWALI:
  Je inakubalika kumuoa Mkiristo atakaesilimu siku ya ndoa? 
 JIBU:
 Sifa
 zote njema anastahiki Allah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah
 na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allahu 'alayhi
 wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na 
watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
 Hakuna
 tatizo lolote endapo atasilimu kidhati, Imepokewa kutoka kwa Anas 
amesema: Abu Twalha alipomuoa Ummu Sulaym, mahari yao ilikuwa ni 
kusilimu, Ummu Sulaym alisilimu mwanzo kabla ya Abu Twalha, 
alipomchumbia, akasema kwa hakika mimi nimeshasilimu, ikiwa utasilimu 
utanioa, akasilimu na ikawa kusilimu ndiyo mahari yao" (An-Nasaaiy 
6/114).
 Lakini
 Muislamu mwanamume awe makini na mwanamke mwenye kutaka kusilimu siku 
ya ndoa, isijekuwa ni mwenye kumdanganya akawa anasubiri siku hiyo 
wakati ameshatayrisha mambo ya harusi kisha amgeukie. Ikiwa hili ndilo 
sharti aliloliweka huyo mwanamke basi nasiha yetu ni kuwa uwe makini na 
ujaribu kuchunguza kwanza dhamira yake. 
 Na Allaah Anajua zaidi
No comments:
Post a Comment