Vipi Aswali Tarawiyh Akiwa Safarini?
SWALI:
Assalam
 alaykum warahmatullah,baada ya salam ya kheri na baraka,nilikua naomba 
kufaham namna ya kuswali taraweh nikiwa safarini,nawatakieni wepesi 
katika kazi zenu,Allah awalipe pepo,amin
JIBU:
Sifa
 zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote,
 Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu
 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) 
na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Muislamu
 anapokuwa safarini ameruhusiwa kupunguza Swalah zake za fardhi, kwa 
hiyo hata Swalah za Sunnah anaweza kuziacha. Yote inategemea na hali 
yake ilivyo huko safarini. Ikiwa unahisi kuwa huwezi kuswali basi ni 
ruhusa kwako, ama ikiwa unao uwezo wa kuswali basi ni vyema kuzitekeleza
 ili upate fadhila na thawabu zake.
 
No comments:
Post a Comment