Mola
 wetu Mtukufu Amemuumba mwanaadamu katika umbo bora lisilomithilika na 
kiumbe chochote. Naye ameumbwa kwa kutumia udongo uliopulizwa roho 
itokayo kwa Mola Mlezi.
 Akamjaalia
 mwanaadamu ni mwenye kupata shida, mitihani, mtenda dhambi na mwenye 
kupata maradhi. Hakusita hapo Mola wetu Mtukufu, bali Akajaalia mlango 
wa pili wa kutokea kwenye mashaka ya dunia; Akajaalia kuwepo starehe, 
utulivu, toba na afya. Basi ni kwa neema zipi mwanaadamu anaweza kumlipa
 Mola wake!?
 Tutambue
 kwamba hii roho tuliyokuwa nayo yatosha kuwa ni sababu ya kushukuru 
neema za Mola Mlezi kwa vitendo na kauli. Tusisahau wapi tulipotoka na 
wapi tunaelekea, hatukuwa chochote miaka 100 iliyopita. Basi ni nani 
kati yetu alikuwa na uhakika kwamba atadhihiri duniani kwa jina na umbo 
lake kabla ya kuzaliwa? Kuwa na adabu kwa kumcha Mola wako!
 Muislamu
 yupo juu ya mgongo wa ardhi akiruzukiwa kila chenye manufaa na yeye, ni
 mwenye kula akapata njia ya kutolea uchafu, na siku uchafu unaposhindwa
 kutoka ndani ya tumbo ndio unaelewa umuhimu wa neema ya kuyeyusha 
chakula kwenye mwili. Ameumba kila kitu kwenye kiwango maalumu, kwani 
tumbo likiyeyusha kupita kiwango, mwanaadamu ataugua maradhi ya tumbo la
 kumuendesha. Hivyo, kumbuka na yazingatie maneno ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
 {{Na mkihesabu neema za Allaah hamtaweza kupata idadi yake. Hakika Allaah ni Mwingi wa kusamehe (na) Mwingi wa kurehemu.}} [An-Nahl: 18]
 Basi
 elewa ndugu yangu, kwamba sisi si chochote si lolote zaidi ya tone la 
manii lililoengwa engwa hadi likafikia miezi tisa likaweza kutoka kwa 
sura ya mwanaadamu. Ndani ya tumbo, Mola wetu Mlezi Alitulinda na wala 
hatukuhitaji askari, jeshi, polisi, ultimate security au mwengineye. 
Ukatoka kwa ukenya wa kilio cha juu ukiomba msaada kwa mama yako. 
Ukafikia baleghe ukaweza kuoa/kuolewa na sasa kwa Qadar ya Mola unaweza 
nawe kupata mtoto. Aliyekuwa mbabe kati yetu azihesabu neema ngapi 
zimepita baina ya kuzaliwa kwake hadi hivi sasa, kisha aangalie ni kwa 
kiwango gani ataweza kuzishukuru neema hizo. SubhaanaLlaah! Yuko umbali 
gani mwanaadamu kwa kuzitilia maanani neema za Mola wake?
 Ugeuze
 uso wako, uangalie mbingu ilivyotanda na ardhi ilivyotandikwa, kisha 
useme kwamba Mola wako amekutupa. Rizki zako Akazimimina kutoka mbinguni
 na Akazichimbua kutoka ardhini. Ni kipi basi katika chakula chako 
kitokacho nje ya mfumo huu? Basi kwa Kiburi Chake Mola Mlezi Anastahiki 
kuyaambia makundi ya wanaadamu na majini:
 {{Enyi
 jamii ya majini na watu! Kama mtaweza kupenya katika mbingu na ardhi 
(ili mkimbie Nisikupateni), basi penyeni (Nikuoneni)! Hamtapenya ila kwa
 nguvu (Zangu. Nikikupeni nguvu hizo mtaweza).}} [Ar-Rahmaan: 33]
 Tumcheni
 Mola wetu kwa kila kitu, kwa dogo na kubwa, kwa tunayoyajua na 
tusiyoyajua. Tutende mema kabla ya kutufika yale yasiyoweza kuhimili 
miili yetu. Wahenga wanatuambia: "Kijua ndi hichi usipouanika utaula 
mbichi."
No comments:
Post a Comment