Historia Ya Waja Wema Kwa Kifupi - Karne Ya kwanza
KARNE YA KWANZA (1H - 99H)
Imefasiriwa Na:
Abu Sumayyah
‘Abdullaah Abu Jaabir (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
‘Abdullaah
 Abu Jaabir bin ‘Amr bin Hazzam bin Tha’labah al-Answaariy al-Khazrajiy 
as-Sulamiy, ni miongoni mwa waliotoa ahadi ya ‘Uqbah. Alihudhuria vita 
vya Badr na alikufa shahidi katika vita vya Uhud.
‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
‘Abdullaah
 bin ‘Abbaas bin ‘Abdul-Muttwalib bin Haashim bin ‘Abd Manaaf 
al-Qurashiy al-Haashimiy, alikuwa ni binamu yake Mtume (Swalla Allaahu 
'alayhi wa aalihi wa sallam) na alikuwa mfasiri wa Qur-aan. Alizaliwa 
miaka mitatu baada ya Hijrah na alikuwa anaitwa ‘Bahari ya Elimu.’ 
Alishiriki katika Jihaad kule Kaskazini mwa Afrika kwenye mwaka 27H na 
alikufa mwaka 68H.
‘Abdullaah bin ‘Amr (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
‘Abdullaah
 bin ‘Amr bin al-’Aasw bin Waail bin Haashim bin Su’ayd bin Sa’d bin 
Sahm as-Sahmi. Yeye na baba yake walikuwa ni Maswahaba. Alikuwa anajua 
kusoma na kuandika na alipata ruhusa kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 
‘alayhi wa aalihi wa sallam) ya kuandika yote yale aliyokuwa 
akiyazungumza Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). 
Alikufa katika mwaka 65H.
‘Abdullaah bin Mas’uwd (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Alikuwa
 Swahaba mkubwa wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), 
‘Abdullaah bin Mas’uwd bin Ghaafil bin Habiyb (Radhiya Allaahu ‘Anhu), 
alikufa katika mwaka 32H huko Madiynah. Az-Zubayr aliongoza Swalah ya 
Janaazah lake na kuzikwa Baqiy’.
Alikuwa
 ni mtu wa sita kusilimu hata kabla ya ‘Umar bin al-Khattwaab (Radhiya 
Allaahu ‘Anhu). Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) 
alimbashiria makazi yake Peponi. ‘Aliy (Radhiya Allaahu ‘Anhu) alitaja 
jambo hii kusema ya kwamba Mtume alimuamuru Ibn Mas’uwd kupanda mti 
kuchuma kitu fulani na kuleta chini. Maswahaba walikuwa wakiangalia 
miundi ya Ibn Mas’uwd wakati akipanda mti na waliaanza kumcheka kutokana
 na uwembamba wa miundi yake. Mjumbe wa Allaah alisema: “Ni kitu gani 
kinachowachekesha? Miguu ya Ibn Mas’uwd ni mizito kwenye mizani siku ya 
Qiyaamah kuliko Mlima Uhud.”
[Imesimuliwa na Imaam Ahmad katika Musnad yake na kuthibitishwa na Shaykh Ahmad Shaakir (920)].
‘Abdullaah
 bin Mas’uwd alikuwa msomaji mkubwa wa Qur-aan. Inasemekana alikuwa ni 
mmoja wa watu wenye kufuata kwa karibu sana muongozo wa Mtume (Swalla 
Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam).
Imekusanywa kutoka kwenye kitabu cha Siyaar A‘laam an-Nubalaa - cha Adh-Dhahabiy na Tahdhiyb At-Tahdhiyb cha Ibn Hajr.
Abu ad-Dardaa (Radhiya Allaahu ‘Ahnu)
Abu 
ad-Dardaa Uwaymir bin Maalik bin Zayd bin Qays al-Khazrajiy 
al-Answaariy. Kuna maoni tofauti kuhusu jina lake. Alisilimu wakati wa 
vita vya Badr na alishuhudia vita vya Uhud. Alikuwa ni Mwanachuoni wa 
Shari’ah. Mchaji Allaah miongoni mwa Swahaba. Alikufa katika mwaka 32H.
Abu Dharr al-Ghifaariy (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Abu 
Dharr al-Ghifaariy Jundub bin Junaadah bin Sakn alikuwa ni miongoni 
waliosimu mwanzoni lakini alichelewa kufanya Hijrah hivyo hakushiriki 
vita vya Badr. Fadhila zake ni nyingi na alikufa mwaka 32H.
Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Abu 
Hurayrah, ‘Abdur-Rahmaan bin Swakhr ad-Dawsiy alikwenda kwa  Mtume kama 
Muhaajir wakati wa vita vya Khaybar. Alihifadhi idadi kubwa ya Hadiyth. 
Zaidi ya Hadiyth elfu nane zilisimuliwa kutoka kwake. Alikufa katika 
mwaka 58H.
Mtume 
Alimuombea du’aa yeye na mama yake kwa kusema: “Ee Allaah! Wajaalie hawa
 waja wako (wawili) ni wenye kupendwa na Waumini na wafanye Waumini ni 
wenye kuwapenda.” [Imesimuliwa na Muslim].
Abu Muwsaa al-Asha’riy (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Abu 
Muwsaa al-Ash’ariy ‘Abdullah bin Qays bin Saalim alikuwa ni mwenye sauti
 nzuri wakati wa kusoma Qur-aan na ni mmoja wa Wanachuoni  miongoni mwa 
Maswahaba. Inasemekana alikufa mwaka wa 42H au 44H.
Abu Sa’iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Abu 
Sa’iyd al-Khudriy Sa’ad bin Maalik bin Sinaan bin ‘Ubayd al-Answaariy 
al-Khazrajiy. Yeye na baba yake wote walikuwa ni Maswahaba na 
alishuhudia vita vyote vilivyofuata baada ya vita vya Uhud. Alikuwa ni 
mmojawapo wa Wanachuoni miongoni mwa Maswahaba na alisimulia Hadiyth 
nyingi za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Alikufa 
katika mwaka 74H.
‘Adiy Bin Haatim (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
‘Adiy 
bin Haatim bin ‘Abdillaah bin Saa’d bin al-Hashraj bin ‘Aamr al-Qays 
at-Twaaiy, Abu Tarif. Alikuwa Mkristo aliyesilimu na kuhudhuria vita vya
 Jamal, Swiffiyn na an-Nahrawaan pamoja na ‘Aliy. Alikufa katika mwaka 
68H.
Al-Bara’a bin Maalik (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Al-Bara’a
 bin Maalik bin an-Nadr al-Answaariy.Alihudhuria vita vya Uhud na alitoa
 ahadi ya utii chini ya mti. Alikufa shahidi katika mwaka wa 20H kwenye 
siku Tustar.
Al-Mughiyrah Bin Shu’bah (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Al-Mughiyrah
 bin Shu’bah bin Abi ‘Aamir bin Mas’uwd ath-Thaqafiy, Abu ‘Abdillaah. 
Alihudhuria vita vya Hudaybiyyah, Al-Yamaamah na alipata ushindi kule 
Syria na Iraq. Alikufa katika mwaka 50H.
‘Amr Bin al-‘Aasw (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
‘Amr 
bin al-’Aasw bin Wa’il al-Qurashiy as-Sahmiy Alisilimu katika mwaka wa 
Sulhu Hudaybiyyah na alikuwa ni mmoja wapo kati ya wale walioshinda  
kule Misr. Alifariki katika mwaka 43H.
Anas Bin Maalik (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Anas 
bin Maalik bin an-Nadr, Abu Hamzah, al-Answaariy, an-Najjaariy. Alikuwa 
mfanyakazi wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). ambaye
 alikaa nae karibu kwa takriban miaka kumi tangu alipohama mpaka kifo 
cha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Alikuwa ni 
miongoni mwa Maswahaba wa mwisho kufariki. Alifariki akiwa na miaka 93H 
kule Baswrah akiwa na miaka 103.
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Alimuombea du’aa kwa kusema: “Ee Allaah Mjalie utajiri na watoto na Vibariki vile ulivyomruzuku.” [Muslim]. 
Na katika mapokezi mengine Anas Aliongezea kwa kusema: “Na
 (kutoka kwa) Allaah fungu langu imekuwa kubwa watoto wangu na wajukuu 
wameongezeka kiasi cha kufikia mia moja kwa kuwahesabu.” [Muslim].
‘Aaishah (Radhiya Allaahu ‘Anha)
‘Aaishah
 bint Abi Bakr (Radhiya Allaahu ‘Anhuma). Mke wa Mtume (Swalla Allaahu 
‘alayhi wa aalihi wa sallam). Baada ya Khadiyjah (Radhiya Allaahu ‘Anha)
 kufariki, Malaika Jibriyl alimuonyesha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa
 aalihi wa sallam) kwenye ndoto kabla ya kumuoa na alikuwa na miaka kumi
 na nane wakati Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) 
alipofariki.
Alifariki katika mwaka 59H kwenye tarehe kumi na saba ya mwezi wa Ramadhwaan. Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘Anhu) alimzika.
Alikuwa
 Mama wa Waumini Asw-Swiddiyqah (Radhiya Allaahu ‘Anha). ‘Umar 
alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Ni nani 
unayempenda zaidi miongoni mwa watu? Akajibu: ‘Aaishah’. Kisha, 
akamuuliza miongoni mwa wanaume (ni nani unayempenda zaidi)? Akajibu: 
Baba yake.”
Ash-Sha’abiy
 alisema: Wakati Masruwuq anatusimulia kuhusu ‘Aaishah, alisema: 
‘Niliambiwa na mkweli, bint wa mkweli, mpendwa miongoni mwa vipenzi vya 
Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Asiye na hatia 
ambaye ndoa yake ilianzishwa kutoka mbingu ya saba.
Az-Zuhriy
 alisema: “Iwapo elimu ya Mama ‘Aaishah itakusanywa na kulinganishwa na 
elimu ya wakeze wengine Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa 
sallam) na wanawake wengine wote basi elimu ya Mama ‘Aaishah ingelibakia
 kuwa isiyo na kifani.”
‘Imran Bin Huswayn (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Imran 
bin Huswayn al-Khuza’iy al-Ka’biy, Abu Nujayd. Alisilimu mwaka wa vita 
vya Khaybar na aliripoti baadhi ya Hadiyth za Mtume (Swalla Allaahu 
‘alayhi wa aalihi wa sallam). Alikufa katika mwaka 52H.
Jaabir Bin ‘Abdillaah (Radhiya Allaahu ‘Anhu)
Jaabir
 bin ‘Abdillaah bin ‘Amr bin Harram al-Answaariy as-Sulamiy. Alishuhudia
 ‘Uqbah wakati wa pili huku akiwa mtoto. Inasemekana alihudhuria vita 
vya Badr na Uhud na kuripoti Hadiyth nyingi za Mtume (Swalla Allaahu 
‘alayhi wa aalihi wa sallam). Alifariki katika Mwaka wa 74H.
allah atujaalie
ReplyDelete