Dunia 
ni tamu na kawaida ya mwanaadamu kupenda mazuri mno. Hujitahidi kadiri 
ya juhudi zake kukusanya yale ayaonayo kuwa ni yenye kufurahisha nafsi 
yake. Hutafuta yale yenye laghai na anasa - 'material world'.
 Hilo
 halina shaka na hata Qur-aan na Sunnah yatuthibitishia kwamba dunia 
imeumbwa kuunganishwa na matamanio ya mwanaadamu. Lakini sio yote ambayo
 Muislamu anatakiwa kuyatilia mkazo kwa kuyavamia. Ndio lengo la kuwepo 
halali na haramu ndani ya Uislamu ili kumtofautisha mwanaadamu na 
Muislamu.
 Waislamu
 walio wengi kabisa wanatamka shahaadah ya kwamba Allaah (Subhaanahu wa 
Ta’ala) ni Mmoja na Ndiye Apaswaye kuabudiwa pamoja na kutiiwa Mtume 
Wake (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kikomo cha wengi 
kinamalizia hapa kwenye kauli tu. Matendo yao
 yanakuwa kinyume na kauli hii. Hivyo, hufanya ibada kwa kudanganya 
macho ya waumini, kwani wanatenda mbele ya kadamnasi, wanapokuwa peke yao huingia kwenye hiyo 'material world' kwa mapana na marefu. Hiyo sio iymaan inayopigiwa mfano na Mola Mlezi:
 {{Ambao wanamuogopa Mola wao (hata) wanapokuwa faraghani, na pia hukiogopa Qiyaamah.}} [21:49]
 Taariykh
 yatufunza kwamba Waislamu hapo kale walilelewa kwenye Tawhiyd ya 
kumuamini Allaah pamoja na Malaika, Mitume, Vitabu, Siku ya Mwisho, 
Qadar kheri na shari. Kwa wakati wa sasa ni Kitabu cha Qur-aan pekee 
ndicho kilicho mbele ya macho yetu. Vilivyobaki vyote vinabaki kuwa 
nyuma ya pazia 'ghayb'.
 Imesimuliwa kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘Anhu): amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwamba: 
 "Iymaan
 ni kumuamini Allaah, na Malaika Wake, na Vitabu Vyake, na Kukutana 
Kwake (Siku ya Qiyaamah), na Mitume Wake na kuamini ufufuo wa Siku ya 
Mwisho." (Imepokewa na Shaykhaan)
 Kukosa
 kuamini moja ya nguzo za iymaan, kunapelekea kutoamini ghayb. Hivyo, 
kuanguka kwa iymaan ya ghayb kutasababisha kuondoka iymaan ya kwamba 
Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Yupo.
 Ni 
ghayb hii inayomfanya mwanaadamu na hata Muislamu kutotilia mkazo 
kuutafuta ukweli halisi wa Uislamu, ghayb ndiko kunakomfanya Muislamu 
kutotenda mema kwa lengo la kupata ridhaa ya Allaah. Thawabu wala dhambi
 hazioni mtu, Malaika wanaoandika mema na maovu nani anayewaona? Haya 
yote yapo kwenye ghayb. Muislamu anatakiwa kuamini hii ghayb bila ya 
mjadala. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anatuambia:
 {{Tendeni
 mambo (mazuri). Allaah Atayaona mambo yenu hayo na Mtume Wake na 
Waislamu. Na mtarudishwa kwa Mjuzi wa siri na dhahiri; Naye Atakwambieni
 (yote) mliyokuwa mkiyatenda.}} [9:105]
 Apambanue
 Muislamu juu ya kukosa kwake iymaan ya ghayb na kuirudisha nyuma akili 
kabla ya kuwepo kwake; yeye alikuwa ni nani? Nani aliyemhifadhi ndani ya
 tumbo la mama kwa miezi tisa? Hivyo, ghayb ni wajibu kuiamini na kwamba
 yapo mambo nyuma ya macho yetu yanatokea au yapo tayari kutokea.
 Kukosekana
 kwa iymaan ya ghayb ndani ya nafsi ya Muislamu ndio kwamfanya awache 
himma ya kutenda mema. Ni sababu hii inayowafanya vijana walio wengi 
kujishughulisha mno na ratiba za mipira inayokula muda wa Waislamu. Nao 
kina dada kutilia mkazo urembo, mikusanyiko ya haramu na kutembea kwao 
utupu kunatokana na kukosa kwao kuamini ghayb. 
 Basi 
na aangalie Muislamu alivyoumbwa, chakula chake kinavyoyayushwa na 
kugaiwa sehemu mbali mbali. Vitamini, damu, madini, sukari, chumvi, 
mafuta na vyengineo; vyote vinapelekwa na kuhifadhiwa sehemu zake 
maalum. Atupe jicho lake kwa kuangalia linapotoka na kuzama jua, tofauti ya usiku na mchana, hali ya uzima na ugonjwa, maisha na mauti na mengineyo: 
 {{Naye
 ndiye Aliyeziumba mbingu na ardhi kwa haki. Na wakati Anaposema 
(kuliambia jambo): "Kuwa," basi huwa… Mjuzi wa ya siri na dhahiri…}} [6:73]
 Basi ni mengi yaliyopo Mkononi Mwako yaa Allaah! Namna tutakavyojifunza katu hatutafikia chembe ya 'ilmu Yako. Hivyo, tunatamka kama ambavyo Umetufunza:
No comments:
Post a Comment