Saturday 28 February 2015

Mambo Matano Uwezayo Kuwafanyia Wazazi Waliofariki Kama Kwamba Wako Hai-1



 Wazazi wetu ni sababu ya kuweko kwetu duniani kwa idhini ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), na kupata radhi zao ni sababu ya kuingizwa kwetu Peponi. Je, anapofariki mmoja wao au wote wawili, ndio mwisho wa kuwatendea wema?
Jibu ni kwamba tunaweza kuendelea kuwatendea wema kama kwamba wako hai tukipata thawabu zetu na wao pia. Baadhi ya amali za kuwatendea zimetajwa katika Hadiyth ifuatayo:
 عن أبي أسيد مالك بن ربيعة رضي الله عنه قال:  بينا نحن جلوس عند رسول الله صلى الله عليه وسلم إذا جاءه رجل من بني سلمة فقال يا رسول الله هل بقي من بر أبوي شيء أبرهما به بعد موتهما ؟ قال: ((نعم! الصلاة عليهما والاستغفار لهما وإنفاذ عهدهما من بعدهما وصلة الرحم التي لا توصل إلا بهما وإكرام صديقهما)) رواه ابن حبان في صحيحه  أبو داود وابن ماجه
Kutoka kwa Abu Asyad Maalik bin Rabiy’ah (Radhiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Tulipokuwa tumekaa pamoja na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi   wa sallam) alikuja mtu kutoka [kabila la] Bani Salamah akasema: Ee Mtume Allaah, ‘Je, kuna kilichobakia katika wema ninaoweza kuwafanyia wazazi wangu baada ya kifo chao? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa Sallam) akajibu, ((Ndio; kuwaswalia [yaani kuwaombea du’aa] kuwaombea maghfirah, kuwalipa deni [au ahadi] zao, na kuunga ukoo ambao hauungiki ila kutokana nao, na kuwakirimu rafiki zao)) [Ibn Hibbaan katika Swahiyh yake, Abu Daawuud na Ibn Maajah]

1-Kuwaswalia (kuwaombea du’aa):
Ni miongoni mwa amali tatu ambazo zinaendelea kumfikia mzazi aliyefariki kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam):
 ((إذا مات إبن آدم إنقطع عمله إلا من ثلاث: صدقة جارية  أو علم ينتفع به أو ولدٌ صالح يدعوا له))  مسلم
((Anapokufa mja, hukatika amali zake zote isipokuwa mambo matatu, swadaqah inayoendelea, au elimu yenye kunufaikiwa, au mtoto mwema anayemuombea)) [Muslim]
Ni amri pia kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anaposema:
 ((وَقُل رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا))
((Na useme: Mola wangu! Warehemu kama walivyonilea utotoni)) [Al-Israa: 23-24]

Hii ni du’aa mojawapo inayopasa kuwaombea, kwa sharti kuwaombea kipekee na si kwa mkusanyiko wa watu. 

Du’aa za kuwaombea wazazi waliofariki kama zilivyokuja katika Qur-aan na Sunnah:

Katika Qur-aan:

 رَّبِّ ارْحَمْهُمَا كَمَا رَبَّيَانِي صَغِيرًا
Rabbir-Hamhumaa kamaa Rabbayaaniy Swaghiyraa.
Mola wangu! Warehemu kama walivyonilea utotoni. [Al-Israa: 24]

رَبَّنَا اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِلْمُؤْمِنِينَ يَوْمَ يَقُومُ الْحِسَاب  
Rabbanagh-fir-liy wa liwaalidayya walil Mu-uminiyna yawma Yaquwmul hisaab.
Mola wetu! Unighufirie mimi na wazazi wangu wote wawili, na Waumini, siku ya kusimama hisabu. [Ibraahiym: 41]
رَبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ  
Rabbigh-fir-liy waliwaalidayya  
Mola wangu! Nighufirie mimi na wazazi wangu. [Nuuh 28]
 رَبِّ اغْفِرْ لِي وَلِوَالِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيْتِيَ مُؤْمِنًا وَلِلْمُؤْمِنِينَ وَالْمُؤْمِنَاتِ  
Rabbigh-fir-liy wa liwaalidayya waliman dakhala baytiya Mu-uminan wa lil Mu-uminiyna wal Mu-uminaati 
Mola wangu! Nighufirie mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wanawake [Nuuh: 28]

Katika Sunnah wanaposaliwa Swalaah ya Janaazah:
Maiti mwanamume
اللهُـمِّ اغْفِـرْ لَهُ وَارْحَمْـه، وَعافِهِ وَاعْفُ عَنْـه، وَأَكْـرِمْ نُزُلَـه، وَوَسِّـعْ مُدْخَـلَه، وَاغْسِلْـهُ بِالْمـاءِ وَالثَّـلْجِ وَالْبَـرَدْ، وَنَقِّـهِ مِنَ الْخطـايا كَما يُنَقَّ الـثَّوْبُ الأَبْيَـضُ مِنَ الدَّنَـسْ، وَأَبْـدِلْهُ داراً خَـيْراً مِنْ دارِه، وَأَهْلاً خَـيْراً مِنْ أَهْلِـه، وَزَوْجَـاً خَـيْراً مِنْ زَوْجِه،  وَأَدْخِـلْهُ الْجَـنَّة، وَأَعِـذْهُ مِنْ عَذابِ القَـبْر وَعَذابِ النّـار
Allaahumma-Ghfir-lahu warhamhu, wa 'aafihi wa’afu 'anhu, wa akrim nuzulahu, wawassi' mudkhalahu, waghsilhu bilmaai wath-thalji walbaradi, wanaqqihi minal-khatwaayaa kamaa yunaqqath-thawbul abyadhwu minad-danas, wa abdilhu daaran khayran min daarihi, wa ahlan khayran min ahlihi, wazawjan khayran min zawjihi, wa adkhilhul-Jannah, wa a’idh-hu min ‘adhaabil-qabri, wa ‘adhaabin-naar  
Eee Allaah, Mghufurie na Mrehemu, na Muafu na Msamehe na Mtukuze kushuka kwake (kaburini) na Mpanulie kuingia kwake, na Muoshe na maji na kwa theluji na barafu na Mtakase na makosa kama inavyotakaswa nguo nyeupe kutokana na uchafu, na Mbadilishie nyumba bora kuliko nyumba yake na jamaa bora kuliko jamaa zake, na mke bora kuliko mke wake, na Muingize Peponi na Mkinge na adhabu ya kaburi (na adhabu ya moto)

Maiti mwanamke:
اللهُـمِّ اغْفِـرْ لَهُا وَارْحَمْـها، وَعافِهاِ وَاعْفُ عَنْـها، وَأَكْـرِمْ نُزُلَـها، وَوَسِّـعْ مُدْخَـلَها، وَاغْسِلْـهُا بِالْمـاءِ وَالثَّـلْجِ وَالْبَـرَدْ، وَنَقِّـهِا مِنَ الْخطـايا كَما يُنَقَّ الـثَّوْبُ الأَبْيَـضُ مِنَ الدَّنَـسْ، وَأَبْـدِلْهُا داراً خَـيْراً مِنْ دارِها، وَأَهْلاً خَـيْراً مِنْ أَهْلِـها، وَزَوْجَـاً خَـيْراً مِنْ زَوْجِها،  وَأَدْخِـلْهُا الْجَـنَّة، وَأَعِـذْهُا مِنْ عَذابِ القَـبْر وَعَذابِ النّـار
Allaahumma-Ghfir lahaa warhamhaa, wa 'aafihaa wa’fu 'anhaa, wa akrim nuzulahaa, wawassi' mudkhalahaa, waghsilhaa bilmaai wath-thalji walbarad, wanaqqiha minal-khatwaayaa kamaa yunaqqath-thawbul abyadhwu minad-danas, wa abdilhaa daaran khayran min daarihaa, wa ahlan khayran min ahlihaa, wazawjan khayran min zawjihaa, wa adkhilhal-jannah, waa’idh-haa min ‘adhaabil-qabri, wa ‘adhaabin-naar

Kuwaombea wazazi wawili:
اللهُـمِّ اغْفِـرْ لَهُما وَارْحَمْـهما، وَعافِهِما وَاعْفُ عَنْـهما، وَأَكْـرِمْ نُزُلَـهما، وَوَسِّـعْ مُدْخَـلَهما، وَاغْسِلْـهُما بِالْمـاءِ وَالثَّـلْجِ وَالْبَـرَدْ، وَنَقِّـهِما مِنَ الْخطـايا كَما يُنَقَّ الـثَّوْبُ الأَبْيَـضُ مِنَ الدَّنَـسْ، وَأَبْـدِلْهُما داراً خَـيْراً مِنْ دارِهما، وَأَهْلاً خَـيْراً مِنْ أَهْلِـهما، وأَزَوْاجَـاً خَـيْراً مِنْ اَزْوَاجِهِما  وَأَدْخِـلْهُما الْجَـنَّة، وَأَعِـذْهُما مِنْ عَذابِ القَـبْر وَعَذابِ النّـار
Allaahumma-Ghfir lahumaa warhamhumaa, wa 'aafihimaa wa’fu 'anhumaa, wa akrim nuzulahumaa, wa wassi' mudkhalahumaa, waghsilhumaa bil maai wath-thalji wal barad, wanaqqihimaa minal khatwaayaa kamaa yunaqqa-th-thawbul abyadhw minad-danas, wa abdilhumaa daaran khayran min daarihimaa, wa ahlan khayran min ahlihimaa, wa azwaajan khayran min azwaajihimaa, wa adkhilhumaal-Jannah, wa a’idh-humaa min ‘adhaabil qabri, wa ‘adhaabin-naar
Maiti zaidi ya wawili
اللهُـمِّ اغْفِـرْ لَهُم وَارْحَمْـهم، وَعافِهِم وَاعْفُ عَنْـهم، وَأَكْـرِمْ نُزُلَـهم، وَوَسِّـعْ مُدْخَـلَهم، وَاغْسِلْـهُم بِالْمـاءِ وَالثَّـلْجِ وَالْبَـرَدْ، وَنَقِّـهِم مِنَ الْخطـايا كَما يُنَقََّ الـثَّوْبُ الأَبْيَـضُ مِنَ الدَّنَـسْ، وَأَبْـدِلْهُم داراً خَـيْراً مِنْ دارِهم، وَأَهْلاً خَـيْراً مِنْ أَهْلِـهم، وأَزَوْاجَـاً خَـيْراً مِنْ اَزْوَاجِهِم  وَأَدْخِـلْهُم الْجَـنَّة، وَأَعِـذْهُم مِنْ عَذابِ القَـبْر وَعَذابِ النّـار
Allaahumma-Ghfir lahum warhamhum, wa 'aafihim wa’fu 'anhum, wa akrim nuzulahum, wawassi' mudkhalahum, waghsilhum bilmaai wath-thalji walbarad, wanaqqihim minal-khatwaayaa kamaa yunaqqath-thawbul abyadhwu minad-danas, wa abdilhum daaran khayran min daarihim, wa ahlan khayran min ahlihim, wa azwaajan khayran min azwaajihim, waadkhilhumul-Jannah, wa a’idh-hum min ‘adhaabil-qabri, wa  ‘adhaabin-naar

Baadhi ya Wema Waliotangulia wametaja kwamba “Atakayewaombea wazazi wake kila siku mara tano (baada ya Swalah za fardhi) atakuwa ametimiza haki zao kutokana na kauli ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
أَنِ اشْكُرْ لِي وَلِوَالِدَيْكَ إِلَيَّ الْمَصِيرُ
((Nishukuru Mimi na wazazi wako. Ni Kwangu Mimi ndiyo marudio)) [Luqmaan: 14]

Na Allaah Anajua zaidi.

2-Kuwaombea maghfirah:
Kila unapowaombea maghfirah wao hupandishwa daraja Peponi:

عن أبي هريرة رضي الله عنه ، قال : قال رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّه عَلَيْه ِ وَ سَلَّمَ: ((إِنَّ الرَّجُلَ لَتُرْفَعُ دَرَجَتُهُ فِي الْجَنَّةِ فَيَقُولُ : أَنَّى هَذَا ؟ فَيُقَالُ :باسْتِغْفَارِ وَلَدِكَ لَكَ)) لإمام أحمد  و في سنن ابن ماجة أيضاً بإسنادٍ صحيح  
Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: ((Hakika mtu hupandishwa daraja yake Peponi. Kisha huuliza: Kwa ajili ya nini? [huku kupandishwa kwangu daraja?] Huambiwa: Kwa ajili ya kuombewa maghfirah na mtoto wako)) Ahmad, na katika Sunan Ibn Maajah ikiwa na isnaad Swahiyh]

Inaendelea…

Nyakati Tatu Muhimu Za Kufanya Ibada – Zisikupite Katika Ramadhaan


Nyakati tatu hizi ni muhimu sana za kufanya ibada kutokana na fadhila zake kuu. Mwenye kupenda kuchuma thawabu nyingi asizikose khaswa katika mwezi huu Mtukufu Wa Ramadhaan ambao ni mwezi wenye malipo maradufu

1-Wakati wa mwanzo:  Baina ya Alfajiri na jua kuchomoza:

Usimulizi uliothibiti kutoka katika Swahiyh Muslim (564/1) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) na Maswahaba walikuwa wakibakia macho wakati huo hadi jua kuchomoza kwani ni wakati mja anapogaiwa rizki yake, na ni wakati wenye kheri nyingi, unampa siha nzuri ya mwili binaadamu, na kwa ujumla ni wakati wenye baraka nyingi za kila aina kwani Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) aliomba: 

((اللهم بارك لأمتي في بكورها))  الترمذي, أحمد, أبي داود, ابن ماجه 
((Ee Allaah, wabarikie Ummah wangu nyakati za asubuhi mapema)) [At-Tirmidhiy, Ahmad, Abu Daawuud, Ibn Maajah na imethibitishwa kuwa ni Hadiyth Swahiyh na Shaykh Al-Albaaniy]

Usimulizi huu umetoka kwa Maswahaba kadhaa ambao wameelezea kwamba: "Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) alipotaka kupeleka kikosi au jeshi aliwapeleka mwanzo wa asubuhi". Vile vile wamesimulia kwamba: "Swakhar alikuwa mtu tajiri ambaye alikuwa akipelekea biashara zake mwanzo wa asubuhi na matokeo yake ilikuwa ni kufuzu katika biashara na kupata faida kubwa sana".

Wamesimulia Salafus-Swaalih kwamba Ibn 'Abbaas naye alimkataza mtu kulala nyakati hizo alipomwambia:

   "قُم، أتنام في الساعة التي تقسَّم فيه الأرزاق؟"
"Inuka! Je, unalala katika saa ambayo rizki inagaiwa?"
Ikiwa wakati huo ni kama hivyo ilivyoelezwa juu, basi vipi Muislamu aache wakati huu umpite hasa katika mwezi huu mtukufu wa Ramdhaan?
Ibnul-Qayyim (Rahimahu-Allaah) katika kitabu chake 'Zaad Al-Ma'aad' amesema: "Usingizi wa asubuhi unanyima rizki kwani huo ni wakati ambao Muumba anaombwa rizki na wakati wa kugaiwa rizki. Hivyo usingizi unanyima rizki isipokuwa kwa dharura. Usingizi wakati huo pia ni madhara kwa mwili…"  


Faida nyingine kubwa ya kubakia macho ukimdhukuru Allaah wakati huu:  

Kwa muda wa saaa moja na nusu takriban utakuwa umepata thawabu za Hajj na ‘Umrah zikiwa kamilifu:
عن أنس عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنه قال  (( من صلى الفجر في جماعة ثم قعد يذكر الله  حتى تطلع الشمس ثم صلى ركعتين كانت له كأجر حجة وعمرة تامة تامة تامة) ) أخرج الترمذي  صححه الألباني .
Imetoka kwa Anas kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: ((Atakayeswali Alfajiri katika Jamaa'ah kisha akakaa anamdhukuru  Allaah mpaka likachomoza jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio kamili kamili kamili)) [Imetolewa na At-Tirmidhiy na kaisahihisha Al-Albaaniy]

Pindi ukifanya hivyo kwa mwezi mzima utakuwa umechuma thawabu za Hajj na ‘Umrah za muda wa mwezi mzima. Hizo ni fadhila za siku za kawaida, seuze ukifanya mwezi mtukufu huu wa Ramadhaan? Jitahidi ndugu Muislamu kadiri uwezavyo kuchuma hizi thawabu kubwa ambazo zingelikukalifu mali, tabu za safari na mashaka ya kufika Makkah kutekeleza ibada hizo. Lakini kwa Rehma ya Allaah Amejaalia thawabu hizo ziweze kuchumwa tukiwa majumbani mwetu tena kwa wepesi kabisa. Wanaume inawapasa waswali msikitini kuzipata thawabu hizo kwa kuwa Hadiyth imetaja atakayeswali jamaa’ah. Ama wanawake, wanazipata fadhila hizo hata wakiswali majumbani mwao. Hata hivyo, juu ya kuweko fadhila kama hiyo, tusisahau kuwa haivunji wala haifuti fardh ya kwenda Hajj kwa mwenye uwezo, asije mtu akadhani kufanya hayo kutakuwa kumetengua wajibu wake wa kuhiji au kufanya ‘Umrah.


2- Wakati wa pili: Kabla ya Jua kuzama (Magharibi):

Huu ni wakati ambao bado Muislamu yuko katika Swawm na du'aa yake anayoiomba hairudi:

 قال صلى الله عليه وسلم: ((ثَلاثةٌ لا تُرَدُّ دعوتُهم: الصَّائم حتَّى يُفْطِر، والإمام العادِل، ودعْوة المظْلوم)) وروى الترمذي  بسند حسن
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: (([Watu] watatu du'aa zao hazirudi; mwenye kufunga Swawm hadi afuturu. Kiongozi muadilifu na aliyedhulumiwa)) [At-Tirmidhiy kwa isnaad nzuri]

Ni fursa kwa Muislamu atumie wakati huo kuomba du'aa wakati huu hasa kwa vile ni wakati ambao Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amehimiza Atukuzwe kama Anavyosema:
 وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ الْغُرُوبِ  
 ... na msabbih kwa kumsifu Mola wako  kabla ya kuchomoza jua na kabla ya kuchwa  [Qaaf: 39]
  
 وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ قَبْلَ طُلُوعِ الشَّمْسِ وَقَبْلَ غُرُوبِهَا وَمِنْ آنَاء اللَّيْلِ فَسَبِّحْ وَأَطْرَافَ النَّهَارِ لَعَلَّكَ تَرْضَى  
 …Na msabbih Mola wako kwa kumsifu kabla ya kuchomoza jua, na kabla halijachwa, na nyakati za usiku pia umsabbih na ncha za mchana ili upate ya kukuridhisha  [Twaahaa: 130].

  وَاسْتَغْفِرْ لِذَنبِكَ وَسَبِّحْ بِحَمْدِ رَبِّكَ بِالْعَشِيِّ وَالْإِبْكَار
Na omba maghfirah kwa dhambi zako, na umsabbih Mola wako  kwa kumsifu jioni na asubuhi)) [Ghaafir: 55]
   
3- Wakati wa tatu: Suhuur - Kabla ya Alfajiri

Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Amewaaahidi wenye taqwa Pepo kwa sababu miongoni mwa sifa zao ni  kuomba maghfira kabla ya Alfajiri: 

 إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَعُيُون. آخِذِينَ مَا آتَاهُمْ رَبُّهُمْ إِنَّهُمْ كَانُوا قَبْلَ ذَلِكَ مُحْسِنِينَ.   كَانُوا قَلِيلًا مِّنَ اللَّيْلِ مَا يَهْجَعُونَ.    وَبِالْأَسْحَارِ هُمْ يَسْتَغْفِرُون.

Hakika wenye taqwa watakuwa katika Jannaat na chemchem. Wanapokea Aliyowapa Mola wao. Kwa hakika hao walikuwa kabla ya haya wakifanya mema. Walikuwa wakilala kidogo tu usiku. Na kabla ya Alfajiri wakiomba maghfira. [Adh-Dhaariyaat: 15-18]



Kisha wamesifiwa tena kwa sifa kama hiyo pamoja na nyinginezo:

 الصَّابِرِينَ وَالصَّادِقِينَ وَالْقَانِتِينَ وَالْمُنفِقِينَ وَالْمُسْتَغْفِرِينَ بِالأَسْحَارِ   
Wanaosubiri, wanaosema kweli, na watiifu, na wanaotoa sadaka, na wanaoomba maghafira kabla ya Alfajiri. [Al-'Imraan: 17]

Muislamu asiache wakati huo umpite kwani ni wakati muhimu na wenye fadhila na faida kubwa kwa vile Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Huteremka wakati huo kutoka mbingu ya saba na kuweko mbingu ya ardhi kututakabalia maombi ya anayemuomba: 

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ: ((يَنْزِلُ رَبُّنَا تَبَارَكَ وَتَعَالَى كُلَّ لَيْلَةٍ إِلَى السَّمَاءِ الدُّنْيَا حِينَ يَبْقَى ثُلُثُ اللَّيْلِ الْآخِرُ يَقُولُ: مَنْ يَدْعُونِي فَأَسْتَجِيبَ لَهُ مَنْ يَسْأَلُنِي فَأُعْطِيَهُ مَنْ يَسْتَغْفِرُنِي فَأَغْفِرَ لَهُ)) البخاري و مسلم  
Imetoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema: (Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Huteremka (kwa namna inavyolingana na utukufu Wake) kila siku katika mbingu ya dunia (mbingu ya kwanza) inapobakia thuluthi ya mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba Nimtakabalie? Nani ana shida Nimtekelezee? Nani ananiomba maghfirah Nimghufurie?)) [Al-Bukhaariy na Muslim]

Nani miongoni mwetu asiyemhitaji Mola wake kumtakabalia haja zake au kumuondeshea shida zake? Nani asiyekuwa na madhambi asiyemhitaji Mola wake kumghufuria? Hivyo usiache wakati huu ukakupita hasa kwa vile ni mwezi wa Ramadhaan ambao kila jambo ulifanyalo lina fadhila na thawabu marudufu.

Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuwezeshe kudiriki nyakati hizo tatu na nyingine, tuwe katika ibada katika mwezi huu wa Ramadhaan na miezi yote mingineyo na Atujaalie kheri na Baraka nyingi, Atutakabalie haja zetu, Atuondoshee shida zetu na Atughufurie madhambi yetu yote. Aamiyn.

15-Rasuli (Swalla Allaahu ‘Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam) Alitilia Umuhimu Mkubwa Kuhusu Tawhiyd

Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alithibitisha Tawhiyd akatoa mafunzo kwa Maswahaba tokea kutumwa kwake kama Rasuli mpaka kufariki kwake. Ikawa Tawhiyd ni jambo kuu akilingania na kupigana vita kwa ajili yake. Alipomtuma Mu’aadh bin Jabal (Radhwiya Allaahu 'anhu) kuwa gavana wa Yemen na Qaadhwiy wao alimwambia: 
((إِنَّكَ تَأْتِي قَوْمًا مِنْ أَهْلِ الْكِتَابِ, فَلْيَكُنْ أَوَّلَ مَا تَدْعُوهُمْ إِلَيْهِ شَهَادَةَ أَنْ لاَ إِلَهَ إِلاَّ اَللَّهُ))
((Unakwenda katika nchi ya watu wa Ahlul-Kitaab, kwa hiyo, jambo la kwanza walinganie katika shahada ya laa ilaaha illa Allaah)). [Al-Bukhaariy, Muslim na wengineo]

Akawafundisha Maswahaba wengineo:
عن أبي عَمْرو، وَقِيلَ: أبي عَمْرَةَ، سُفْيَانَ بْنِ عَبْدِ اللهِ  رَضيَ اللهُ عَنْهُ قَال: قُلْتُ: يا رَسُولَ الله، قُلْ لي في الإِسْلاَمِ قَوْلاً، لاَ أَسْأَلُ عَنْهُ أَحَداً غَيْرَكَ. قَال: ((قُلْ: آمَنْتُ باللهِ ثُمَّ اسْتَقِمْ)).  
Kutoka kwa Abu 'Amru vile vile (anajulikana kama) Abu 'Amrah Sufyaan bin ‘Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: “Nilisema: Ee Rasuli wa Allaah, niambie kitu kuhusu Uislamu ambacho siwezi kumuuliza mtu yeyote isipokuwa wewe.  Akasema: ((Sema; Namuamini Allaah, kisha kuwa mwenye msimamo)). [Muslim]

Watoto pia aliwfundishwa Tawhiyd:

 

عَنْ أبي العَبَّاس عَبْدِ اللهِ بنِ عَبَّاسٍ رَضي اللهُ عنهما قال: كُنْتُ خَلْفَ النَّبِيِّ صلى الله عليه وسلم يًوْماً، فقال: ((يا غُلامُ، إنِّي أُعَلِّمُكَ كلِماتٍ: احْفَظِ اللهَ يَحْفَظْكَ، احْفَظِ اللهَ تَجِدْهُ تُجاهَك، إذا سأَلْتَ فاسْأَلِ اللهَ، وإذا اسْتَعنْتَ فاسْتَعِنْ باللهِ، واعْلَمْ أنَّ الأُمَّة  لَوِ اجْتَمَعَتْ على أَنْ يَنْفَعُـوكَ بِشَيءٍ لَمْ يَنْفَعُوكَ إلا بِشَيْءٍ قدْ كَتَبَهُ اللهُ لَكَ، وإن اجْتَمَعُوا على أن يَضُرَّوكَ بِشيءٍ لَمْ يَضُروكَ إلا بِشَيءٍ قَدْ كَتَبهُ اللهُ عَلَيْكَ، رُفِعَتِ الأقْلامُ وَجَفَّتِ الصُّحُفُ))
Kutoka kwa Abul ‘Abbaas ‘Abdullaah bin ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: “Siku moja nilikuwa nyuma ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: ((Ee kijana! Nitakufundisha maneno (yenye manufaa); Mhifadhi Allaah Atakuhifadhi. Muhifadhi Allaah na utamkuta mbele yako. Ukiomba, muombe Allaah, ukitafuta msaada tafuta kwa Allaah. Tambua kwamba, ikiwa ummah mzima utaungana kukunufaisha wewe kwa kitu, basi hutonufaika ila tu kwa kile Alichokwishakuandikia Allaah, na wakikusanyika kukudhuru kwa chochote, hotodhurika ila tu kwa kile Allaah Alichokwishakuandikia (kuwa kitakudhuru), kwani Kalamu zimeshanyanyuliwa na sahifa zimeshakauka (Majaaliwa yasiyobadilikika). [At-Tirmidhiy akasema ni Hadiyth Hasan Swahiyh]   
 

Mpaka katika hali ya kufariki kwake alitilia umuhimu mkubwa Tawhiyd:

عَنْ عَائِشَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهَا قَالَتْ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ فِي مَرَضِهِ الَّذِي لَمْ يَقُمْ مِنْهُ: ((لَعَنَ اللَّهُ الْيَهُودَ وَالنَّصَارَى اتَّخَذُوا قُبُورَ أَنْبِيَائِهِمْ مَسَاجِدَ))
Kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa): Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema alipokuwa katika maradhi ambayo hakuinuka tena [alipokaribia kufariki]: ((Allaah Amewalaani Mayahudi na Manaswara wamegeuza makaburi ya Mitume yao kuwa Misikiti)). [Al-Bukhaariy na Muslim na wengineo]

Nabiy Ya’quwb (‘Alayhis-Salaam) naye pia aliwausia wanawe akiwa karibu ni kufariki kwake:

أَمْ كُنتُمْ شُهَدَاءَ إِذْ حَضَرَ يَعْقُوبَ الْمَوْتُ إِذْ قَالَ لِبَنِيهِ مَا تَعْبُدُونَ مِن بَعْدِي قَالُوا نَعْبُدُ إِلَـٰهَكَ وَإِلَـٰهَ آبَائِكَ إِبْرَاهِيمَ وَإِسْمَاعِيلَ وَإِسْحَاقَ إِلَـٰهًا وَاحِدًا وَنَحْنُ لَهُ مُسْلِمُونَ ﴿١٣٣﴾
Je, mlikuwa mashahidi wakati mauti yalipomfikia Ya’quwb alipowaambia wanawe: “Mtaabudu nini baada yangu?” Wakasema: “Tutamwabudu Ilaah (Muabudiwa wa haki) wako na Ilaaha wa baba zako, Ibraahiym na Ismaa’iyl na Is-haaq; Ilaah Mmoja (Pekee) nasi Kwake tunajisalimisha (katika Uislamu).” [Al-Baqarah: 133]

Namna Ya Kujikinga Kunapotokea Fitnah

Namna Ya Kujikinga Kunapotokea Fitnah

Katika wakati wa fitnah, ni waajib Muislamu kufanya yafuatayo:

1.   Kujishughulisha na kutafuta elimu ya Dini.

2.   Kujishughulisha na kumuabudu Allaah (Tabaaraka wa Ta'alaa); mambo haya yatamlinda na fitnah.

Kadhaalika, kujikinga na fitnah kunapatikana kwa kufanya yafuatayo:

1.   Kushikamana na Qur-aan na Sunnah.

2.   Kujishughulisha sana na kumfanyia 'Ibaadah Allaah (Tabaaraka wa Ta'alaa)


3.   Kuwa na ukaribu na maingiliano na watu wema.

4.   Kukaa mbali na watu waovu.

5.   Kujiweka mbali na maeneo maovu, na vilevile kujiweka mbali na mambo yenye kupelekea katika maovu.

Shaykh 'Abdul-'Aziyz Ar-Rajihiy (Hafidhwahu-Allaah),
Sharh Uswuwl As-Sunnah, uk. 147.