Wednesday 29 July 2015

Complete Mp3 Al Qur'an 30 Juz - Syeikh Maher Al Muaiqly

Rudi Tena Ukaswali, Kwani Hukuswali


Imefasiriwa na Ilyaasa Mawlaana


Kwa jina la Allaah, Mwingi wa Rehma, Mwenye Kurehemu.


Sehemu Ya Kwanza

Katika usiku wa giza, Abu Lu’lu’ Al-Majuusi (kipenzi cha Mashia) alijificha katika vivuli akijiandaa kwa ajili ya Swalaah ya Alfajiri, wakati ambapo ataendesha mipango yake ya kishetani kumuua Amiyr wa waumini – ‘Umar bin Al-Khattwaab (Radhiya Allahu ‘anhu).

‘Umar (Radhiya Allahu ‘anhu) alikuwa (na kawaida) ya kuongoza Swalah ya Alfajiri huku akisoma surah ndefu, akiwapa wafuasi wa jamii, muda wa kuhudhuria mkusanyiko (wa Swalaah). Katika siku hii, wakati (‘Umar) akisoma (Qur-aan), Abuu Lu’Lu’ akachukua hatua kutoka kwenye nguzo inayofifia, hali ya kuwa ana kisu cha sumu katika mkono wa vazi lake. Akaruka mbele ya ‘Umar (Radhiya Allahu ‘anhu) na akamkata tumbo wazi kwa (kile) kisu. Baada ya hapo, akajaribu kuukimbia mkusanyiko. Akiwa ana chana chana mbele na nyuma, akiwauwa watu wengi zaidi ambao walikuwepo katika njia yake. Swahaabah mmoja akamtupia nguo juu yake na alipo tahayari kwamba keshakamatwa Abu Lu’lu’ akajiua. 
‘Abdur-Rahmaan bin ‘Awf (Radhiya Allahu ‘anhu) akaikamilisha Swalaah ya Alfajiri ambayo aliianza ‘Umar (Radhiya Allahu ‘anhu). ‘Umar (Radhiya Allahu ‘anhu) alikamilisha Swalaah yake hali ya kuwa ni miongoni mwa watu (maamuma) katika Jama’ah na akafariki dunia baadaye katika kitanda chake, (Radhiya Allaahu ‘anhu).

Umuhimu wa Swalaah katika Uislamu hauwezi kudharauliwa. Ni nguzo ya kwanza ya Uislamu iliyotajwa na Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) baada ya tamko la Imani (shahaadah), ambayo kutokana nayo mtu huwa Muislamu.

Swalaah imefaradhishwa kwa Manabii na watu wote. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Alitangaza hadhi yake ya kuwa ni faradhi katika tukio Tukufu. Kwa mfano, Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Alipozungumza na Muusa (‘Alayhis Salaam), Amesema:

{{Nami nimekuteua wewe; basi sikiliza unayofunuliwa. Hakika Mimi ndiye Allaah. Hapana muabudiwa wa haki ila Mimi tu. Basi niabudu Mimi, na ushike Swalah kwa ajili ya kunikumbuka Mimi}} [Twaaha: 13-14]

Hivyo hivyo, Swalaah imefaradhishwa kwa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakati alipopelekwa mbinguni. Zaidi, wakati Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anawasifu waumini kama katika Suratul-Al-Mu-uminuun, moja katika sifa ambazo Anazitaja kuhusiana nao ni kule kushikana kwao na Swalaah:
{{Hakika wamefanikiwa Waumini. Ambao ni wanyenyekevu katika Swalah zao}} [Al-Mu’minuun: 1-2]

Umuhimu wa Swalaah unaendelea kuonyeshwa katika kauli nyingi za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kwa mfano, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kasema:

“Jambo la kwanza ambalo mja atahukumiwa katika Siku ya Hisabu ni Swalaah. Kama ikiwa ni nzuri basi amali zake zilizobakia zitakuwa nzuri. Na ikiwa ni mbaya, basi amali zake zilizobakia zitakuwa mbaya.” [At-Twabaraaniy].
Kwa kweli, ikiwa Swalaah imeswaliwa vizuri ikiambatana na ukumbusho  wa kweli wa kumkumbuka Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala), na kumgeukia Yeye kutaka msamaha, itakuwa na athari kubwa juu ya mtu kwa kipindi  kirefu. Mtu anapokamilisha Swalaah yake, moyo wake utajaa ukumbusho wa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). Atakuwa ana hofu na pia vilevile matarajio juu ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). Baada ya tukio hilo, hatotaka tena kuondoka kutoka katika sehemu hiyo ya fakhari kuelekea kwa ile ambayo ndani yake atamuasi Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) anaitaja hali hii ya Swalaah katika Qur-aan:  

{{Hakika Swalah inazuilia mambo machafu na maovu}} [Al-‘Ankabuut: 45].

Lakini katika wale ambao wanaoswali, utakuta kuna vitendo vya kivivu ambavyo vinahitaji kumulikwa. Kwa mfano:

·         Wengine hawazingatii kile ambacho wanakisema.
·         Wengine wanafanya haraka katika Swalah zao
·         Wengine wanaachilia nadhari yao ya macho izurure wakati wa Swalah
·         Wengine mara kwa mara husahau nambari ya rakaa zilizotimizwa.
·         Dunia inakumbatia mioyo ya baadhi ya watu wakati wa Swalah na inafunika akili zao.
·         Na watu wengine katika Jamaa’ah wanaanza kusujudu kabla hata ya Imaam kusema “Allaahu Akbar”

Linganisha hii (hali yetu katika Swalaah) na Swalaah za watu ambao walikuja kabla yetu. Watu walikuwa wanafikiria ya kwamba Ar-Rabiy’ bin Khaytham alikuwa ni kipofu kwa sababu ya kuinamisha macho yake mara kwa mara. Alikuwa akiishi nyumbani kwa Abdullaah bin Mas’uud (Radhiya Allahu ‘anhu) kwa miaka ishirini na mtumwa wake wa kike akimuona alikuwa akisema: “Rafiki yako kipofu anakuja” na Abdullaah alikuwa akimcheka kwa kauli yake.

Ndani ya Al-Bukhaariy na Muslim, Abuu Hurayrah (Radhiya Allahu ‘anhu) anatueleza ya kwamba, kuna mtu aliingia msikitini, ambao Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa amekaa. Akaswali rakaa mbili na kisha akaja kwa Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na akatoa salamu. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaijibu salamu yake na halafu akasema, “Rudi tena ukaswali kwani hukuswali.” Hivyo, yule mtu akarudi, akaswali (rakaa mbili) kama alivyofanya mara ya kwanza, akaja tena na kurudia kutoa salamu. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akaijibu salamu na akasema “Rudi tena ukaswali kwani hukuswali.” Hivyo, yule mtu akarudi, akaswali (rakaa mbili) kama alivyofanya mara ya kwanza akaja tena na kurudia kutoa salamu. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alijibu salamu kwa mara nyingine tena na kwa mara nyingine tena akasema: “Rudi tena ukaswali kwani hukuswali”. Hadi kufikia mara hii ya tatu, mtu huyo alisema: “Naapa kwa Yule ambaye alikutuma wewe na ukweli, Ewe Mtume wa Allaah, sijui vyovyote isipokuwa hivi, Nifundishe.” Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:

“Ikiwa unasimama kwa ajili ya Swalaah sema “Allaahu Akbar”. Halafu soma ambacho kitakujia kwa wepesi katika Qur-aan. Kisha rukuu mpaka utakapohisi kwamba umetulia katika rukuu yako. Kisha, simama mpaka uwe umesimama wima kisawa sawa. Kisha, sujudu mpaka uwe umetulia katika sujudu yako. Kisha keti mpaka uwe umetulia katika juluus yako. Kisha sujudu mpaka uwe umetulia katika sujudu yako. Na uwe unafanya hivi ndani ya Swalaah yako yote”.


(Kwahiyo turudi tukarudie Swalah zetu)

Kwanini tunakuja msikitini; nini sababu yetu ya kutekeleza Swalah? Tunafanya hivyo kwa kufuata amri ya Muumba wetu (Subhaanahu wa Ta’ala). Kwanini hasa tupoteze baraka na thawabu kwa sababu ya moyo usiotulia na mkono unaowasha. Khushuu ni kiini cha Swalaah zetu. Khushuu ni matunda ya imani yetu. Lakini, hata baada ya kujua haya, watu hawafanyi juhudi kukamilisha Swalah zao na kwa hiyo huandikiwa sehemu ndogo tu. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema;

“Kwa hakika, mtu ataondoka (katika Swalaah yake) na ataandikiwa (thawabu) kumi za Swalaah yake; tisa, nane, saba, sita, tano, nne, tatu, nusu.” [Abu Daawuud na at-Tirmidhiy]


‘Uthmaan bin Abii Dahshah (Radhiya Allahu ‘anhu) alisema: “Sijawahi kuswali Swalah ambayo baada yake nilikosa kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anisamehe kwa upungufu wangu katika Swalah ile.”

Mtu ambaye anaharakisha Swalah yake ni mwizi.  Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema katika Hadiyth sahihi, “Mwizi muovu kuliko wote ni yule ambaye anaiba katika Swalaah yake”. Swahaaba (Radhiya Allaahu ‘anhum) wakauliza: “Ewe Mjumbe wa Allaah, anaibaje katika Swalah yake?” Naye (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Hakamilishi rukuu na sujudu zake”


Kwa sababu ya kasi ya jinsi ya watu wanavyoswali, wanaonekana kama ndege, wanaodonoa juu na chini. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikataza  mtu kudonoa (katika Swalah) kama kunguru.


‘Umar (Radhiya Allahu  ‘anhu) wakati mmoja alisimama katika Minbari akiuhutubia umati wa watu kwa sauti ya nguvu akisema, “Mtu anaweza akakulia mpaka utu uzima katika Uislamu na asiweze kamwe kukamilisha kwa ajili ya Allaah hata Swalah moja!” (Watu) wakasema, “Vipi hali hii?” (‘Umar) (Radhiya Allahu ‘anhu) akasema: “Hakamilishi khushuu yake, hata unyenyekevu wake, hata nadhari yake juu ya Allaah ‘Azza wa Jalla.”

Wakati mmoja, Ma’aruuf Al-Karkhiy (Rahimahu Allaah) aliposimama miongoni mwa wanafunzi wake, mmoja wao akamwambia mwenziwe, “Tafadhali swalisha Swalaah ya ‘Ishaa”. Mwanafunzi wa kwanza akakubali lakini akasema “Nitaswalisha Swalaah ya ‘Ishaa kwa sharti ya kwamba wewe utaswalisha Swalaah ya Alfajiri sio mie” Ma’aruuf Al-Karkhiy alishtushwa na kauli aliyoisema na akasema, “Naapa kwa Allaah, ikiwa unafikiria ya kwamba utakuwa hai wakati wa Alfajiri, basi naapa kwa Allaah, hujakamilisha Swalah yako”.


Sehemu Ya Pili

Jinsi ya kuwa na Khushuu ndani ya Swalah
Al-Qaasim bin Muhammad (Rahimahu Allaah) alisema: “Nilikwenda nje siku moja, na kila nilipotoka ni lazima nipite kwa mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allahu ‘anha) na kumsalimia. Siku hiyo nilitoka na nilipomkuta mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allahu ‘anha) akiswali Swalah ya Dhwuhaa, akisoma tena na tena Aayah ya Allaah:
 
{{Tulikuwa zamani pamoja na ahali zetu tukiogopa (adhabu ya Allaah). Basi Allaah Akatufanyia hisani na Akatulinda na adhabu ya Moto.}} [Atw-Twuur: 26-27]

Alikuwa analia na akimwomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na huku akirudia Aayah hiyo. Nilisimama pale mpaka nikachoka, hali ya kuwa yeye amebaki kama nilivyomkuta. Nilipoona haya nilijiambia, “Hebu niende sokoni, nifanye ninachotakiwa kufanya, halafu nije tena”. Kwa hiyo, baada ya kumaliza kufanya nilichotaka kufanya sokoni, nilirudi kwa mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhiya Allahu ‘anha). Alikuwa kama nilivyomuacha, akirudia Ayaah, akimuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na akilia”.
 

Vipi tuwe na khushuu katika Swalaah?

Katika Sunnah ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam)tunafundishwa yafuatayo:


1.     Njoo mapema kwa ajili ya Swalaah na jitayarishe kuwa na khushuu.
Fuatiliza adhana pamoja na Mu’adhin na baada ya adhana, sema dua iliyoamriwa. Omba dua baina ya Adhaana na Iqaamah. Tia wudhuu vizuri, hali ukisukutuwa mdomo wako, na vaa nguo zako nzuri kabisa.

2.     Nuia kupata dhawabu zote za Swalaah yako.
Abu Bakr bin ‘Iyaash alisema, “Nilimuona Habiyb bin Thaabit katika sujudu. Ukimuona utadhania kwamba kashakufa (kwa urefu wa sujudu zake).”


3.     Zingatia Aayah na adhkaar ambayo inasomwa ndani ya Swalaah.
Fikiria kuhusu maana za Aayah ambazo unazisoma. Je haivunji moyo ya kwamba mtu anaweza kuswali miaka kumi baada ya kumi, siku baada ya siku na pia bado hajui anasema nini? Qur-aan iliteremshwa ili itafakariwe! Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Kateremsha (katika Qur-aan Ayaah inayosema):

{{Na hiki Kitabu, Tumekuteremshia wewe, kimebarikiwa, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili.}} [Swaad: 29].


4.     Swali Jama’ah. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anaamrisha:

{{Na simamisheni Swalah, na toeni Zakaah, na rukuuni pamoja na wenye kurukuu.}} [Al-Baqarah: 43].


5.     Usikose kamwe kuswali Swalah zako za nawaafil (Sunnah zilizotiliwa mkazo), hasa zile ambazo Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiswali siku zote, kama vile Witri na Sunnah ya Alfajiri.


6.     Usiharakishe Swalah yako.

Chukua muda wako na usikubali kuifanya Swalah yako kuwa kitendo kilichokuwa hakina thamani katika siku yako. Ibn Wahb (Rahimahu Allaah) alisema: “Nilimuona Ath-Thawriy (Rahimahu Allaah) kwenye Kaa’bah.  Baada ya Swalah ya Magharibi, alinyanyuka kuswali na kisha akasujudu. Hakunyanyuka katika ile sujudu mpaka adhana ya ‘Ishaa ilipoadhiniwa.”


7.     Jua ya kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anajibu Swalah yako. Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema:

“Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Aliyetukuka alisema: “Nimeigawa Swalah kati Yangu na mja Wangu  katika nusu mbili, na mja Wangu atapata alichokiomba” [Kutoka katika Surat ul- Faatiha ] Wakati mja anaposema, “Sifa njema zote ni za Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala), Mola wa viumbe vyote,” Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema, “Mja Wangu Amenihimidi” . Wakati mja anaposema “Mwingi wa Rehema, Mwenye Kurehemu.” Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema, “Mja wangu Amenisifu.” Wakati mja anaposema, “Mwenye Kumiliki Siku ya Malipo”, Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema mja Wangu Amenitukuza”.  Wakati mja anaposema, “Wewe tu tunakuabudu na wewe tu tunakuomba msaada.” Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) anasema, Hii ni kati Yangu Mimi na mja Wangu, na mja Wangu atapata alichokiomba”. Wakati mja anaposema “Tuongoze katika njia iliyonyooka, njia ya  uliowaneemesha, sio ya wale uliowakasirikia, wala ya wale waliopotea,” Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala)  Anasema, “Hivi vyote ni kwa ajili ya mja Wangu, na mja Wangu atapata alichokiomba” [Muslim]


8.     Swali pamoja na kizuizi (weka sutrah) mbele yako na swali karibu yake.

Kitu chengine ambacho kitakusaidia kuwa na khushuu’ [utulivu] ni kushughulika (au kuwa makini) katika suala la kuwa na kizuizi (sutrah) na kuswali karibu yake. Kuwa na sutrah kutazuia uoni wako, kutakulinda juu ya Shaytwaan, na kutazuia watu kupita mbele yako, kitu ambacho husababisha wasiwasi na hupunguza thawabu za Swalah. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: 

“Ikiwa mmoja wenu ataswali basi na aswali akielekea kwenye sutrah, na awe karibu nayo” [Abuu Daawuud].


9.     Tafuta ulinzi] kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) kutokana na Shaytwaan.

Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alitufundisha vipi tupambane na wasi wasi wa Shaytwaan. Abul- ‘Aas (Radhiya Allahu ‘anhu) kasimulia ya kwamba alisema, “Ewe Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Shaytwaan ananisumbua wakati ninaswali, na hupata wasiwasi katika kisomo changu.” Mjumbe wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema, “Huyo ni Shaytwaan  ambaye jina lake ni Khanzab. Ikiwa utahisi kwamba yupo, jilinde kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) kutokana naye, na tema mate (makavu) katika upande wako wa kushoto mara tatu”. Abu’l –‘Aas (Radhiya Allahu ‘anhu) alisema: “nilifanya hivyo na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Akaniondoshea.” [Muslim].

10.            Swali kama kwamba umeambiwa kuwa baada kumaliza Swalah utarudi kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). Abu Bakr Al-Muzaniy (Rahimahu Allaah) alisema, “Kama unataka Swalah yako ikufae, basi sema: “Nitakufa baada tu ya Swalah hii!”  

Kumuoa Mkristo Atakayesilimu Siku Ya Ndoa



SWALI:
 Je inakubalika kumuoa Mkiristo atakaesilimu siku ya ndoa?
 

 
 
JIBU:
 
 
Sifa zote njema anastahiki Allah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Hakuna tatizo lolote endapo atasilimu kidhati, Imepokewa kutoka kwa Anas amesema: Abu Twalha alipomuoa Ummu Sulaym, mahari yao ilikuwa ni kusilimu, Ummu Sulaym alisilimu mwanzo kabla ya Abu Twalha, alipomchumbia, akasema kwa hakika mimi nimeshasilimu, ikiwa utasilimu utanioa, akasilimu na ikawa kusilimu ndiyo mahari yao" (An-Nasaaiy 6/114).
Lakini Muislamu mwanamume awe makini na mwanamke mwenye kutaka kusilimu siku ya ndoa, isijekuwa ni mwenye kumdanganya akawa anasubiri siku hiyo wakati ameshatayrisha mambo ya harusi kisha amgeukie. Ikiwa hili ndilo sharti aliloliweka huyo mwanamke basi nasiha yetu ni kuwa uwe makini na ujaribu kuchunguza kwanza dhamira yake.
 
Na Allaah Anajua zaidi
 
 

Yajue Mambo Anayopaswa Kufanyiwa Mtu Akifariki


Yampasa Muislam ajiandae kufikiwa na mauti kwa kukithirisha (kufanya sana) matendo mema na kujiepusha na makatazo (vilivyoharamishwa). Vilevile mauti yawe akilini mwake, kwa maneno ya Mtume صلي الله عليه وآله وسلم:
“Zidisheni kukumbuka kiondoshacho ladha (yaani mauti)”. Hadiyth hii imepokewa na Imaam at-Tirmidhiy na akaithibitisha usahihi wake Imaam al-Albaaniy katika kitabu chake Irwaaul-Ghaliyl uk. 682.

Anapofariki Muislam yampasa yule au wale waliopo pale karibu na maiti kumfanyia mambo yafuatayo:
1.     Kuyafumba macho ya maiti huyo kwani Mtume صلي الله عليه وآله وسلم aliyafumba macho ya Abu Salamah alipofariki kisha akasema: “Hakika macho yanafuata roho inapotolewa”. Imesimuliwa na Imaam Muslim.

2.     Avilainishe viungo vya maiti ili visikakamae.

3.     Aifunike maiti hiyo kwa nguo ambayo itasitiri mwili mzima kwa kauli ya mama wa waumini ‘Aaishah:“Hakika alipofariki Mtume صلي الله عليه وآله وسلم alifunikwa kwa nguo iliyomsitiri kote.” Imesimuliwa na Imaam al-Bukhaariy na Imaam Muslim.

4.     Waharakishe kuiandaa maiti, kuiosha, kuikafini, kuiswalia na kuizika. Kwani Mtume صلي الله عليه وآله وسلم amesema: “Liharakisheni jeneza…” Imesimuliwa na Imaam al-Bukhaariy na Imaam Muslim.

5.     Waizike katika mji au eneo alilofia kwa vile katika vita vya Uhud “Mtume صلي الله عليه وآله وسلم aliamrisha mashahidi wa vita wazikwe pahala pale walipofia wala wasihamishwe”. Imepokewa na Ahlus Sunan (Ma-Imaam Abu Daawuud, an-Nasaaiy, at-Tirmidhiy, Ibnu Maajah) na ameithibitisha usahihi wa Hadiyth hiyo Imaam al-Albaaniy katika kitabu chake cha Ahkaamul Janaaiz uk. 14.
 

Ayyuwb: Mfano Katika Imani Na Subira (Ustahimilivu)


Imetafsiriwa na Ukht Haliymah ‘Abdullaah

Historia ya Ayyuwb (katika ujira) inawapa faraja wale wote ambao ni wagonjwa au walionyimwa mali au watoto.
Malaika walikuwa wanajadili hali ya binaadamu, utiifu na uasi wao.
Mmoja wao akasema kwamba Ayyuwb ndio mbora wa watu ulimwenguni. Alikuwa Muumin mtiifu, daima akiswali kwa ajili ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Alimbariki kwa kuwa tajiri miaka themanini. Muda wote huu hakusahau kumuabudu au kumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). Alishirikiana katika utajiri wake na maskini na kuwavisha walio uchi.
Shaytwaan hakuamini kwamba kuna mtumishi mkweli kama Ayyuwb. Shaytwaan alifikiri kwamba utajiri wake ndio sababu ya ukweli wake, kwa hiyo akamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) kwa uwezo Wake amuondoshee Ayyuwb utajiri kwa nia mbaya ya kumpotosha. Allaah Akamuondoshea kumpima Nabii Wake.
Akaonyesha kutokana na upotevu huo kwa kusema utajiri ni wa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) na namshukuru kwa Aliyoniruzuku na namshukuru kwa Aliyochukua. Akashuka chini kwa kusujudu. Hili lilimfanya Shaytwaan akasirike.
Shaytwaan alijaribu mara mbili kumpoteza Ayyuwb baada ya kukosa utajiri wake kwa kumuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) kwa nguvu zake kumuondoshea watoto na afya. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Alisema nitakupa uwezo katika mwili wake, lakini nakutahadharisha kuifikia roho yake, ulimi, moyo, kwa sababu ndani yake inasema uongo kuhusu Imaan ya kweli. Ayyuwb akaonyesha mwenendo alioufuata wakati alipochukuliwa utajiri wake.
Shaytwaan aligundua kwamba hawezi kumpoteza Ayyuwb, hivyo alimwendea mkewe kumpoteza (kumdanganya), kwa kumkumbusha maisha yao ya zamani (ya utajiri). Shaytwaan alifanikiwa katika kumdanganya mkewe. Hilo lilimpelekea kumlalamikia Ayyuwb kuhusu hali waliyo nayo sasa. Hili lilimfanya Ayyuwb kuapa kwamba atampiga viboko 100 ikiwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala ) Atamrudishia afya yake. 
Shaytwaan hakufanikiwa katika kumpoteza Ayyuwb. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Akarudishia vyote Alivyopoteza. Ikabakia kwa Ayyuwb sasa kutimiza kiapo chake cha kumpiga fimbo mkewe.
Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Akamuagiza kumpiga mkewe kwa mara moja fimbo 100 za mianzi, kwa Kumuonea huruma huyo mama. Kweli Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) ni mwingi wa rehema.
Kisa cha Ayyuwb kitakuwa daima ni ukumbusho kwetu sote. Inatakiwa tusome kisa hiki mara kwa mara kwa ajili ya kujikumbusha. Wengi wetu tunalalamika kwa kitu kidogo katika maisha. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Alimpa mtihani Ayyuwb kwa namna ambayo kweli inatakiwa tujihusishe nayo.
Imani yake na uvumilivu ni kitu ambacho kama sisi ni Waumini wa Kiislamu wa kweli tujaribu na kutekeleza katika maisha yetu, wakati Akitupa mtihani katika hali hizi. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) katika Qur-aan:
“…Bila shaka tulimkuta ni mwenye subira, mja mwema, kwa hakika alikuwa mnyenyekevu sana.” Swaad: 44

Wakati huu ni lazima tumkumbuke Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) zaidi, kufanya ibaada kwa bidii, na kuwa wenye kushukuru sana badala ya kutoridhika na hali zetu. Inabidi Tumtukuze na Tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) kwa kila hali Atakayotupa majaribio. Kama tunavyojua huu ni wakati ambao Shaytwaan anajaribu kuchezea akili zetu, hisia, na udhaifu wetu. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Hawezi kusahau kamwe kumlipa mwenye kumtumikia kwa hiyo kazi kubwa.



Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala):
“Na (Mtaje) Ayyuwb alipomwita Mola wake (akasema) Mimi imenipata dhara Nawe Ndiye Unayerehemu kuliko wote wanaorehemu.
“Basi tukamkubalia (wito wake) na tukamuondolea dhara aliyokuwa nayo, na tukampa watu wake na mfano wao pamoja nao. Ni rehma inayotoka Kwetu, na ukumbusho (mzuri) kwa wafanyao ibaada) Al-Anbiyaa: 83-84.
Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Atupe imaan na uvumilivu wakati wa mitihani, Aamiyn.

Mawaridi Kumi Ya Kupata Mapenzi Ya Allaah

 سبحانه وتعالى Na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم


 
 
 
WARIDI LA: 1
 
Omba Tawbah sana kwa Allaah سبحانه وتعالى   Na  jiweke katika Twaharah daima
}}...إِنَّ اللّهَ يُحِبُّ التَّوَّابِينَ وَيُحِبُّ الْمُتَطَهِّرِينَ{{
{{…… Hakika Allaah huwapenda wanao tubu na huwapenda wanao jisafisha}}
Al-Baqarah:222 
 

WARIDI LA:  2 
 Mfuate Mtume صلى الله عليهو آله  وسلم   kwa kutimiza Sunnah zake na fuata tabia na mwendo wake  ili  uthibitishe  mapenzi yako kwa Allaah سبحانه وتعالى
 
}}قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَاللّهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ    {{
{{Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allaah basi nifuateni mimi, Allaah Atakupendeni na atakufutieni madhambi yenu. Na Allaah ni Mwenye kufuta madhambi na Mwenye kurehemu}}
Al-Imraan:31
 
Vile vile  fuata  Sunnah za Makhalifa Wanne waliongoka, Abubakar, 'Umar, 'Uthmaan na 'Aliy
عنهما  رضي الله

WARIDI LA : 3
Timiza Fardhi yako kwanza vizuri, kisha ongeza na Sunnah zaidi za Swalah, kutoa sadaqa, kwenda Umra, kufanya kila aina ya wema kwa wazazi na Waislamu wenzako
((‏عن ‏ ‏أبي هريرة رضي الله عنه ‏ ‏قال ‏
‏قال رسول الله ‏ ‏صلى الله عليه وآله وسلم ‏ ‏إن الله قال ‏ ‏من عادى لي وليا فقد ‏‏ آذنته ‏‏ بالحرب وما تقرب إلي عبدي بشيء أحب إلي مما افترضت عليه وما يزال عبدي يتقرب إلي بالنوافل حتى أحبه فإذا أحببته كنت سمعه الذي يسمع به وبصره الذي يبصر به ويده التي يبطش بها ورجله التي يمشي بها وإن سألني لأعطينه ولئن استعاذني لأعيذنه وما ترددت عن شيء أنا فاعله ترددي عن نفس المؤمن يكره الموت وأنا أكره مساءته))
 
((Inatoka kwa Abu Hurayrah رضي الله عنه ambaye alisema: Mtume ‏صلى الله عليه وآله وسلم  amesema: Hakika Allaah Amesema: Yeyote yule afanyae uadui kwa walii (rafiki) wangu nitatangaza vita dhidi yake.  Mja wangu hanikaribii na kitu chochote ninachokipenda kama amali nilizomuwajibisha, na mja wangu huzidi kunikaribia kwa amali njema za Sunnah ili nimpende. Ninapompenda huwa (Mimi ni) masikio yake anayosikilizia, macho yake anayoonea, mikono yake anayopigania, miguu yake anayokwendea, lau angeniomba kitu bila shaka ningempa, lau angeniomba himaya bila shaka ningempa, sisiti juu ya kitu chochote kama ninavyosita  (kuichukua) roho ya mja wangu muumin.  Anachukia mauti nami nachukia kumuumiza.))
 
(Al-Bukhariy)
 

WARIDI LA:  4
 
Fanya mema mengi Allaah Aridhike na wewe na wewe uridhike na uwe tayari kuondoka duniani hali ya kupenda kwenda kuonana naye.
 
((عن ‏ ‏أبي بردة ‏ ‏عن ‏ ‏أبي موسى ‏
‏عن النبي ‏ ‏صلى الله عليه وآله وسلم ‏ ‏قال ‏ ‏من أحب لقاء الله أحب الله لقاءه ومن كره لقاء الله كره الله لقاءه))
((Kutoka kwa Abu Musa kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  kasema:  Atakayependa kuonana na Allaah basi Allaah Naye Atapenda kuonana naye, na atakayechukia kuonana na Allaah, basi Naye Allaah Atachukia kuonana naye))
 (Muslim)
 

WARDI LA:   5
 
Ukipendwa na Allaah سبحانه وتعالى basi utapendwa na Jibriyl na wakaazi wa mbinguni na watu wa duniani pia
 
((عن ‏ ‏أبي هريرة ‏
‏عن النبي ‏ ‏صلى الله عليه وآله وسلم ‏ ‏قال ‏ ‏إذا أحب الله العبد نادى ‏ ‏جبريل ‏ ‏إن الله يحب فلانا فأحببه فيحبه ‏ ‏جبريل ‏ ‏فينادي ‏ ‏جبريل ‏ ‏في أهل السماء إن الله يحب فلانا فأحبوه فيحبه أهل السماء ثم يوضع له القبول في الأرض))
((Imetoka kwa Abu Hurayrah kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  amesema: AllaahAkimpenda mja Wake) Humuita Jibriyl na Husema: Nampenda fulani kwa hivyo (nawe) mpende.  Kisha Jibriyl humpenda.  Kisha Jibriyl huwaita wakaazi  wa mbinguni: Hakika Allaah Anampenda fulani basi na nyinyi mpendeni.  Basi hupendwa na wakaazi  wa mbinguni, kisha kupendwa kwake hujengwa duniani))
(Al-Bukhariy)
 

WARIDI LA:  6
 
Fanya wema, toa sadaka, jizuie na ghadhabu, wasamehe wenzako wanapokukosea  upate daraja ya Muhsiniyn na upendwe na Allaah سبحانه وتعالى    
}}الَّذِينَ يُنفِقُونَ فِي السَّرَّاء وَالضَّرَّاء وَالْكَاظِمِينَ الْغَيْظَ وَالْعَافِينَ عَنِ النَّاسِ وَاللّهُ يُحِبُّ الْمُحْسِنِينَ{{
{{Ambao hutoa wanapo kuwa na wasaa na wanapo kuwa na dhiki, na wanajizuia ghadhabu, na wasamehevu kwa watu; na Allaah huwapenda wafanyao wema}}
 
(Al-'Imraan 134)
 

WARDI LA: 7
 
 Penda kusoma Suratul-Ikhlaas upate mapenzi ya Allaah سبحانه وتعالى 
 
((عن ‏ ‏أنس ‏أن رجلا قال والله إني لأحب هذه السورة ‏ ‏قل هو الله أحد ‏ ‏فقال رسول الله ‏صلى الله عليه وآله وسلم ‏‏ حبك إياها أدخلك الجنة
الترمذي وصححه الألباني
 
Imetoka kwa Anas ambaye alisema: Mtu mmoja alimwambia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم "Mimi naipenda sura hii  قُلْ هُوَ اللَّهُ أَحَد akasema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  “Mapenzi yako kwayo yatakuingiza peponi”
 
At-Tirmidhiy na  Imesahihishwa na Albaaniy
(Hapa tufahamu kuwa Suratu Ikhlaas ni sehemu ya Qur’an, na ni vizuri kuisoma Qur’an yote na usitosheke na Surah moja au baadhi na ukaacha zingine kwa kuichukua hadiyth hiyo peke yake bila kutazama na zingine).
 

WARIDI LA: 8
  Mpende Allaah سبحانه وتعالى  , Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  na Makhalifa wake wote Wanne Abubakar, 'Umar, 'Uthmaan na ‘Aliy رضي الله عنهما  upate kuwa nao.
 
((عن ‏ ‏أنس ‏ ‏رضي الله عنه ‏
‏أن رجلا سأل النبي ‏ ‏صلى الله عليه وآله وسلم ‏ ‏عن الساعة فقال متى الساعة قال وماذا أعددت لها قال لا شيء إلا أني أحب الله ورسوله ‏ ‏صلى الله عليه وسلم ‏ ‏فقال ‏ ‏أنت مع من أحببت قال ‏ ‏أنس ‏ ‏فما فرحنا بشيء فرحنا بقول النبي ‏ ‏صلى الله عليه وسلم ‏ ‏أنت مع من أحببت
‏قال ‏ ‏أنس ‏ ‏فأنا أحب النبي ‏ ‏صلى الله عليه وسلم ‏ ‏وأبا بكر ‏ ‏وعمر ‏ ‏وأرجو أن أكون معهم بحبي إياهم وإن لم أعمل بمثل))
((Imetoka kwa Anas ‏رضي الله عنه ambaye alisema:
Alikuja mtu mmoja akamuuliza Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  kuhusu saa (Qiyaamah) akauliza: Lini Qiyaamah? Akamuulize je, Kwani umekitayarishia nini?  Akasema: sikutayarisha kitu isipokuwa mimi nampenda Allaah na Mtume wake صلى الله عليه وسلم
Akasema: basi wewe uko pamoja na unayempenda.  Anas akasema: Hatukufurahiwa na jambo kama tulivyofurahiwa na usemi huu wa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم "wewe uko pamoja na unayempenda" Akasema Anas: "Basi mimi nampenda Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na Abu Bakr, na 'Umar na natumai niwe pamoja nao kwa mapenzi yangu juu yao japo kama sikufanya kama walivyofanya wao"))
 
(Al Bukhariy)
 

WARIDI LA: 9
 
Kuwa na Tawakkul katika mambo yako yote, umuweke Allaah سبحانه وتعالى   mbele ya kila jambo, na unapotaka kufanya jambo, kwanza tafuta ushauri kwa watu wema, kisha swali istikhaara, kisha Tawakkal kwa Allaah سبحانه وتعالى   
 
}}شَاوِرْهُمْ فِي الأَمْرِ فَإِذَا عَزَمْتَ فَتَوَكَّلْ عَلَى اللّهِ إِنَّ اللّهَ يُحِبُّ الْمُتَوَكِّلِينَ{{
 
{{ Shauriana nao katika mambo. Na ukisha kata shauri basi mtegemee Allaah. Hakika Allaah huwapenda wanaomtegemea}}
 
Al-Imraan: 159
 

WARIDI LA: 10
 
Kuwa na tabia njema na watu kama, upole, ukarimu, heshima, ucheshi, adabu nzuri upate kuwa karibu na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم siku ya Qiyaamah.
  (( عن أبي جده ‏أنه سمع النبي ‏ ‏صلى الله عليه وآله وسلم ‏ ‏يقول ‏ ‏ألا أخبركم بأحبكم إلي وأقربكم مني مجلسا يوم القيامة فسكت القوم فأعادها مرتين ‏ ‏أو ثلاثا ‏ ‏قال القوم نعم يا رسول الله قال أحسنكم خلقا))
(احمد) 
((Imetoka kwa Abi Jidduh   kwamba amemsikia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akisema:  Je, nikujulisheni nani kipenzi kwangu na nani atakayekuwa karibu yangu siku ya Qiyaama?  Wakanyamaza watu wote, akarudia mara mbili au tatu, wakasema watu: "ndio ewe Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema: mwenye tabia njema katika nyinyi))
(Ahmad)