Wednesday 15 February 2017

Ipi hekma ya kulala upande wa kulia kamaalivyofundisha Mtume Muhamady

Nini Hikma Ya Kulala Upande Wa Kulia Kama Alivyotufundisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم ?

Yote tunayoyapata kutoka katika Sunnah ya mwalimu wetu, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni mafunzo yenye faida kwetu ima faida ya nafsi zetu au faida katika mwili wetu au faida katika maisha yetu na kwa ujumla, bali kuna hikma kubwa kwenye mafunzo hayo:
عن البراء بن عازب رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه و قال صلى الله عليه وسلم : ((إذا أتيت مضجعك فتوضأ وضوءك للصلاة ثم ثم اضطجع على شقك الأيمن ثم قل :  أللهم  أَسْـلَمْتُ نَفْـسي إِلَـيْكَ، وَفَوَّضْـتُ أَمْـري إِلَـيْكَ، وَوَجَّـهْتُ وَجْـهي إِلَـيْكَ، وَأَلْـجَـاْتُ ظَهـري إِلَـيْكَ، رَغْبَـةً وَرَهْـبَةً إِلَـيْكَ، لا مَلْجَـأَ وَلا مَنْـجـا مِنْـكَ إِلاّ إِلَـيْكَ، آمَنْـتُ بِكِتـابِكَ الّـذي أَنْزَلْـتَ وَبِنَبِـيِّـكَ الّـذي أَرْسَلْـت"   واجعلهن آخر كلامك فإن مت مت على الفطرة)) – البخاري و مسلم
Kutoka kwa Al-Baraa Bin 'Aazib رضي الله عنهما kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kasema; utakapofika wakati wa kulala, tawadha kama wudhuu wa Swalah, kisha lala upande wako wa kulia, kisha sema:  "Allaahumma aslamtu nafsiy Ilayka, wa fawwadhwtu amriy Ilayka, wa wajjahtu wajhiya Ilayka, wa aljaatu dhwahriy Ilayka, raghbatan wa rahbatan Ilayka, laa maljaa wa laa manjaa Minka illa Ilayka, aamantu bi-Kitaabikal-ladhiy Anzalta, wa bi-Nabiyyikal-ladhiy Arsalta"
[Ewe Allaah,  nimeisalimisha nafsi yangu Kwako, na nimekuachia mambo yangu Wewe na nimeuelekeza uso wangu Kwako na nimeutegemeza mgongo wangu Kwako, kwa matajarajio na kwa kukuogopa, hapana sehemu ya kukimbilia wala ya kujiokoa ila Kwako, nimekiamini kitabu Chako Ulichokiteremsha na Mtume Wako Uliyemtuma] Na fanya hivyo iwe ni maneno yako ya mwisho kwani utakapokufa utakufa katika Fitwrah [(Uislamu]))  [Al-Bukhaariy na Muslim] 
Hatuna shaka na tunaamini  na kuyafuata  mafunzo yake kadiri tuwezavyo  kwani nani msemaye kweli kuliko Allaah (Subhanaahu wa Ta’ala) na Mjumbe Wake Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)? Mjumbe ambaye hasemi kwa matamanio yake ila ni wahyi utokao kwa Mola wetu Muumba Anayesema:
((وَمَا يَنطِقُ عَنِ الْهَوَى))  (( إِنْ هُوَ إِلَّا وَحْيٌ يُوحَى))
((Wala hatamki kwa matamanio)) ((Hayakuwa haya ila ni ufunuo ulio funuliwa)) [An-Najm: 3-4]

Basi hebu tuone hikma ya kutufunza kulala upande wa kulia.



  

Ubongo (Brain)

 
Ubongo sehemu yake huwa upande wa kulia na ndio ambao unauongoza Moyo ulioko upande wa kushoto.


Mapafu (Lungs)



Pafu la upande wa kulia wa mwili ni kubwa kuliko pafu la upande wa kushoto, kwa kuwa pafu la upande wa kulia lina sehemu 3 wakati ambapo la upande wa kushoto lina sehemu 2 tu.
Ini (Liver)

   
Ini liko upande wa kulia na ndilo tezi (gland) kubwa kubwa kabisa mwilini.


Nyongo (Gall Bladder)


 
Nyongo nayo nipo upande wa kulia na ina majukumu ya kutengeneza utomvu ambao unameng’enyua (digest) mafuta.

 
 
Matumbo (Intestines)


 

Matumbo (Intestines) Na Sehemu Ya Mwisho Wa Utumbo (colon)

 


Sehemu ya 'mwisho wa Utumbo mkubwa' (colon) na mwisho wa matumbo (intestines) yako upande wa kulia. (Appendix) 
 
 
Moyo 
 

Moyo uko upande wa kushoto na ndio pampu la taratibu ya mzungukuo(circulatory system)
Tumeona kwamba  kwamba viungo vya mwili vikubwa viko upande wa kulia katika mwili, kwa hiyo mtu anapolala upande wa kushoto, huathiri viungo hivi na huleta madhara katika siha ya Binaadamu. Na juu ya hivyo mtu anapolala upande wa kulia huwa haileti shinikizo katika vyumba vya mapumziko ya moyo ambazo hufanya wepesi kazi ya Taratibu ya Mzunguko (circulatory cycle).
Kwa hiyo mtu anayelala upande wa kulia anapoamka asubuhi huamka akiwa mwenye nguvu na  mchangamfu.
Hadiyth za  Mtume صلى الله عليه وآله وسلم tulizoamrishwa na mapendekezo ya kulala upande wa kulia

عن أبي  هريرة رضي الله عنه قال :" رأى رسول الله صلى الله عليه و سلم رجلاً مضطجعاً على بطنه فقال ((إن هذه ضجعة يبغضها الله و رسوله))". رواه الترمذي  .
Imetoka kwa Abu Hurayrah رضي الله عنه ambaye kasema: Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alimuona mtu amelala kifudifudi, akasema: ((Kulala huku kunachukizwa na Allaah سبحانه وتعالى na Mtume Wake)) [At-Tirmidhy]

  عن  عائشة أن رسول الله  صلى الله عليه وسلم   "كان   إذاصلى  ركعتي    الفجر    (يعني سنتها)  اضطجع على شقه   الأيمن"  - صحيح البخاري
Imetoka kwa mama wa waumini 'Aaishah رضي الله عنها  kwamba "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  akishaswali rakaa mbili za Alfajiri, [yaani Sunnah za Alfajiri]  hulala upande wa kulia" [al-Bukhaariy] 
  


عن أبي أمامة قال: مر النبي صلى الله عليه وسلم على رجل نائم في المسجد منبطح على وجهه فضربه برجله وقال: (( قم أو اقعد فإنها نومة جهنمية))
 مسند أحمد وسنن ابن ماجه
Kutoka kwa Abu Amaamah kasema; alipita Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kwa mtu mmoja ambaye alikuwa amelala kifudifudi  msikitini akampiga hivi (teke) kwa mguu akasema: ((Inuka au kaa kwani kulala huku ni kama kulala kwa watu wa motoni))   [Musnad Ahmad na Sunan Ibn Maajah]

وعن حفصة رضي الله عنها قالت:" كان النبي صلى الله عليه وسلم إذا أخذ مضجعه جعل يده اليمنى تحت خده الأيمن" رواه الطبراني، صحيح الجامع  
Kutoka kwa mama wa waumini Hafswah رضي الله عنها   ambaye kasema: "Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alikuwa anapotaka kulala huweka mkono wake katika shavu la kulia" [At-Twabraaniy katika Swahiyh al-Jaami'y]
Amesema Imaam Ibn al-Qayyim (Allaah Amrehemu): "Kulala kwake Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa ubavu wake wa kulia kuna siri, nayo ni kuwa Moyo unakuwa juu kwa upande wa kushoto, kwa hivyo, ikiwa atalalia ubavu wake wa kushoto basi usingizi utakuwa mzito; kwani atakuwa katika hali ya utulivu na ushwari na hivyo kuwa usingizi wake ni mzito. Na kama atalala kwa upande wa ubavu wake wa kulia, basi atakuwa katika hali ya wasiwasi na usingizi wake utakuwa si mzito kwa kuwa moyo utakuwa katika hali ya wasiwasi na atahitajia utulie na moyo kupondokeka kwake.

1 comment:

Mymovies said...

Absolutely posting! Lots of useful information and inspiration, both of which we all need!Relay appreciate your work.
quran-translation-in-urdu