Wednesday 17 June 2015

TAQABBALA ALLAAHU MINNAA WA MINKUM - FAIDA MBALIMBALI ZA RAMADHWAAN


Assalaamu 'alaykum wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh,
ALHIDAAYA inawaombea Ramadhwaan ya kheri na Baraka nyingi, mchume thawabu tele, Swawm zikubaliwe, dhambi zighufuriwe, na Allaah Atutakabalie 'amali zetu.  
Tusiache kuwaombea du’aa ndugu zetu Waislam popote walipo ulimwenguni walio katika dhiki za ukandamizwaji, vita, njaa na machafuko. Na pia tukumbukane kwa du’aa kwani Mtume Swalla-Allaahu alayhi wa aalihi wa sallam amesema katika Hadiyth kutoka kwa Ummu Dardaa Radhwiya-Allaahu ‘anhaa: ((Atakayemuombea ndugu yake kwa siri Malaika aliyewakilishwa kwake husema: “Aamiyn nawe pia upate mfano wake)) (wa kama unayomuombea) [Muslim] 
Kwa Munaasabah wa mwezi mtukufu wa Ramadhwaan, Alhidaaya imewaekea tayari mafundisho mbalimbali yenye manufaa katika kuongeza elimu na kuimarisha 'ibaadah zenu ili muweze kuchuma mema mengi na muweze kufikia kuipata taqwaa ambayo ndio lengo kuu la Swawm. 

No comments: