Saturday 11 April 2015

Anajitegeme Mwenyewe, Anachangia Katika Futari, Je Anawajibika Kutoa Zakaatul-Fitwr?

SWALI:
salam alaykum.
Swali langu ni kwamba. Mimi nataka kutoa zaka ni msichana ninae jitegemea lakini nimekua nafturu kwa ndugu tofauti mwezi mzima. Na pia huko ninako enda kufuturu nachanigia kitu katika ftar. Je zakaah yangu niitoe vipi?
Waaleykum saam.



JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Kufuturu kwa watu au kuchangia futari haihusiani na hukmu ya kutoa Zakaatul-Fitwr kwani hikma ya kutoa Zakaatul-Fitwr ni kuitwaharisha Swawm ya mwenye kufunga kutokana na maneno maovu, machafu ambayo ameyatamka. Vile vile ili kuwapatia masikini nao chakula kizuri siku ya 'Iyd nao wafurahi. Dalili ifuatayo ni uthibitisho:     
عَنْ ابْنِ عَبَّاس ٍقَالَ فَرَضَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ زَكَاةَ الْفِطْرِ طُهْرَةً لِلصَّائِمِ مِنْ اللَّغْوِ وَالرَّفَثِ وَطُعْمَةً لِلْمَسَاكِينِ مَنْ أَدَّاهَا قَبْلَ الصَّلاةِ فَهِيَ زَكَاةٌ مَقْبُولَةٌ وَمَنْ أَدَّاهَا بَعْدَ الصَّلاةِ فَهِيَ صَدَقَةٌ مِنْ الصَّدَقَاتِ . " رواه أبو داود  بِإِسْنَادٍ حَسَنٍ .

Kutoka kwa Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) ambaye amesema: "Mtume amefaridhisha Zakaatul-Fitwr kuwa ni twahara ya mwenye kufunga kutokana na maneno ya upuuzi na machafu, na kulisha masikini. Atakayeitoa kabla ya Swalah basi hiyo ni Zakaah iliyotakabaliwa, na atakayeitoa baada ya Swalah basi hiyo ni Sadaqah miongoni mwa Sadaqah" [Abu Daawuud kwa isnaad iliyo nzuri].

Kwa hiyo  ni waajib wako kuota Zakaatul-Fitwr maadam una uwezo na unajitegemea mwenyewe.

Kwa maelezo zaidi bonyeza kiungo kifuatacho upate kusoma mas-ala  mbalimbali yanayohusu Zakaatul-Fitwr:


Na Allaah Anajua zaidi
 

No comments: