Saturday 11 April 2015

Vipi Aswali Tarawiyh Akiwa Safarini?


SWALI:
Assalam alaykum warahmatullah,baada ya salam ya kheri na baraka,nilikua naomba kufaham namna ya kuswali taraweh nikiwa safarini,nawatakieni wepesi katika kazi zenu,Allah awalipe pepo,amin



JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.

Muislamu anapokuwa safarini ameruhusiwa kupunguza Swalah zake za fardhi, kwa hiyo hata Swalah za Sunnah anaweza kuziacha. Yote inategemea na hali yake ilivyo huko safarini. Ikiwa unahisi kuwa huwezi kuswali basi ni ruhusa kwako, ama ikiwa unao uwezo wa kuswali basi ni vyema kuzitekeleza ili upate fadhila na thawabu zake.

Na Allaah Anajua zaidi

No comments: