Tuesday 25 August 2015

Ukumbusho Wa Swiyaam (Funga) za Ayyaamul-biydhw (Masiku meupe) Dhul-Qa'dah 1436H

SWIYAAM (FUNGA) SIKU TATU KILA MWEZI THAWABU ZAKE NI SAWA NA THAWABU ZA SWIYAAM YA MWAKA!
Tunapenda kuwakumbusha Swiyaam (funga) za Ayyaamul-biydhw (masiku meupe) ambayo ni tarehe 13, 14, 15 katika kila mwezi wa Kiislaam (Hijriyyah). Masiku hayo mwezi huu wa Dhul-Qa’dah 1436H, yataangukia tarehe 28, 29, 30 August (Ijumaa, Jumamosi, Jumapili). Bonyeza 'Endelea' upate fadhila kadhaa za Ayyaamul-biydhw na fadhila za Swiyaam siku tatu kila mwezi, pamoja na fadhila za Swiyaam kwa ujumla.  Soma  na utekeleze ili ufaidike na ujichumie thawabu tele In Shaa Allaah.  Na hakuna tawfiyq isipokuwa ya Allaah ‘Azza wa Jalla, Kwake tunatawakali na Kwake tunarudia kutubia.

Nasiha Za Minasaba Mbali Mbali

Tumeingia Katika Miezi Mitukufu Inatupasa Kuitakasa Kwa Kuacha Maovu Na Kuzidisha Mema

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):
((إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللّهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللّهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَات وَالأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ذَلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ فَلاَ تَظْلِمُواْ فِيهِنَّ أَنفُسَكُم))

((Hakika idadi ya miezi kwa Allaah ni miezi kumi na mbili katika hukumu ya Allaah, tangu Alipoumba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko minne mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo)) [At-Tawbah: 36].

Miezi minne hiyo imetajwa katika Hadiyth ifuatayo:
  عَنْ أَبَى بَكْرَة أَنَّ رَسُول اللَّه - صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ - قَالَ فِي حَجَّة الْوَدَاع : ((إِنَّ الزَّمَان قَدْ اِسْتَدَارَ كَهَيْئَتِهِ يَوْم خَلَقَ اللَّه السَّمَوَات وَالْأَرْض السَّنَة اِثْنَا عَشَر شَهْرًا مِنْهَا أَرْبَعَة حُرُم : ثَلَاث مُتَوَالِيَات ذُو الْقَعْدَة وَذُو الْحِجَّة وَالْمُحَرَّم وَرَجَب مُضَر الَّذِي بَيْن جُمَادَى وَشَعْبَان)) صَحِيح الْبُخَارِيّ

No comments: