Tuesday 25 August 2015

Wasiya Wa Pili Wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) – Swalaah Ya Adhw-Dhwuhaa.

Imetajwa pia katika Hadiyth ya Abu Ad-Dardaai kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amemuusia naye mambo matatu kama aliyomuusia Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu), nayo ni: Swiyaam (kufunga) siku tatu, kuswali Swalaah ya adhw-dhwuhaa na kuswali Swalaah ya Witr kabla ya kulala,
وعَنْ أَبِي الدَّرْدَاءِ رضي الله عنه قَالَ : "أَوْصَانِي حَبِيبِي صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ بِثَلَاثٍ لَنْ أَدَعَهُنَّ مَا عِشْتُ : بِصِيَامِ ثَلَاثَةِ أَيَّامٍ مِنْ كُلِّ شَهْرٍ، وَصَلَاةِ الضُّحَى  وَبِأَنْ لَا أَنَامَ حَتَّى أُوتِرَ"   رواه مسلم  
Imepokelewa kutoka kwa Abu Ad-Dardaai (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba: “Ameniusia mpenzi wangu Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam [mambo] matatu nisiyaache maishani mwangu; Swiyaam (kufunga) siku tatu kila mwezi na Swalaah ya Adhw-Dhwuhaa na nisilale mpaka niswali Witr” [Muslim]

Swalaah ya Adhw-Dhwuhaa – Fadhila zake, idadi ya raka’ah zake na wakati wake:

No comments: